Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amegundua ujanja unaofanywa na baadhi ya wananchi wa Moshi mkoani Kilimanjaro wa kutochukua hati miliki za ardhi kwa lengo la kukwepa kulipa kodi ya ardhi.

Kufuatia hali hiyo Lukuvi ameagiza takriban hati 5,000 ambazo hazijachukuliwa katika Wilaya hiyo kuchukuliwa na wahusika na watakaoshindwa kuzichukua watafikishwa mahakamani kwa kosa la kukwepa kulipa kodi. Katika Manispaa ya Moshi Jumla ya viwanja 15,000 vimepimwa na kati ya hivyo ni hati 10,168 tu ndizo wamiliki wake wamejitokeza kuzichukua.

Aidha, Waziri Lukuvi amemuagiza Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi katika wilaya ya Moshi mkoa wa Kilimanjaro kuhakikisha ifikapo februari mwaka ujao (2019) anasitisha kesi za migogoro ya ardhi na kuanza kujikita katika kusikiliza kesi za wamiliki wa ardhi wasiolipa kodi ya ardhi ili kuiwezesha serikali kupata mapato.

‘’Wote wasiolipa kodi iwe waliokuwa na hati ama wasio na hati lakini wanaishi katika maeneo ya mijini yaliyopangwa ikifika februari 2019 watafikishwa mahakamani na tutahakikisha wanadaiwa kuanzia kipindi walichomilikishwa na wakishindwa nyumba zao zitapigwa mnada’’ alisema Lukuvi

Akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo zaidi ya 150 waliojitokeza kuwasilisha kero zao za ardhi kwa Waziri Lukuvi katika program maalum ya Funguka kwa Waziri leo (jana), alisema katika ziara yake wilayani Moshi amebaini kuna hati zipatazo 5000 huku baadhi yake zikiwa na zaidi ya miaka 18 hazijachukuliwa na wahusika ambapo kwa mujibu wa Lukuvi wengi wao hawataki kuzichukua kwa kuogopa kulipa kodi ya ardhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...