Na Editha Shija-Tabora

Mganga mkuu (DMO) wa halmashauri ya wilaya ya nzega mkoani Tabora Dk,Edward Sengo anatuhumiwa kutumia Lugha za kuudhi na kutotoa ushirikiano kwa viongozi na watendaji wa kata ,hali inayoelezwa kusababisha kuwa inadhoofisha huduma za Afya wilayani humo

Tuhuma hizo zilitolewa Jana na diwani wa kata ya Nkiniziwa Angelina Simon Kisasembe katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano ya halmashauri hiyo

Aidha diwani huyo alisema,Mganga huyo amekuwa akikwamisha jitahada na utoaji wa huduma bora za Afya katika kata hiyo kutokana na kauli zake zisizokuwa na mantiki nzuri katika jamii.

Aliongeza kwa kusema kuwa DMO ni kiongozi wa mfano mzuri katika kitengo cha huduma za Afya katika wilaya hiyo kwani anapaswa kushirikiana vizuri na madiwani na watendaji wa kata zote

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Said Shemahonge alipotakiwa kulitolea ufafanuzi jambo hilo alisema kuwa hana taarifa yoyote ile ya malalamiko yanayoelekezwa kwa mtumishi huyo ila aliahidi kulifanyia kazi na atatoa taarifa kwa kikao kijacho cha baraza.
Baadhi ya Madiwani wakiwa kwenye kikao hicho cha Balaza la Madiwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...