Mbunifu wa mavazi vyota nchini, Doreen Peter Noni anayetamba na lebo ya Eskado Bird ameibuka na kipindi maalum cha televisheni kijulikanyo kwa jina la ‘Tena Na Tena’ ambacho kinazungumzia shughuli mbalimbali za kutafuta riziki katika maisha mpaka kufanikiwa.

Akizungumza na gazeti hili jana, Doreen ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu na Mwanzilishi na mmiliki wa kituo cha redio, Lake FM cha Mwanza alisema kuwa, sababu kubwa ya kuanzisha kipindi hicho ambacho kitarushwa katika moja ya vituo vya televisheni hapa nchini mwakani, ni kutoa hamasa kwa vijana kuendelea ‘kupambana’ katika kutafuta riziki bila kukata tamaa.

Doreen alisema kuwa kipindi cha Tena na Tena ambacho pia kitaonyeshwa ‘Online’, kimerekodiwa kwenye gari inayotembea ambapo muhusika atatoa ushuhuda wake wa maisha katika mfumo wa majadiliano. Alisema kuwa mbali ya kuburudisha, lengo lingine la kipindi cha Tena na Tena ambacho kitaanza kurushwa hewani hivi karibuni ni kutoa elimu kwa vijana katika kukabiliana na changamoto za maisha.


Mbunifu wa Mavazi na Mkurugenzi wa Kituo Cha Redio cha Lake FM, Doreen Peter Noni akirekodi kipindi cha Tena na Tena na wasanii Nevi Kenzo

 Mbunifu wa Mavazi na Mkurugenzi wa Kituo Cha Redio cha Lake FM, Doreen Peter Noni akirekodi kipindi cha Tena na Tena na msanii Vanessa Mdee
  Mbunifu wa Mavazi na Mkurugenzi wa Kituo Cha Redio cha Lake FM, Doreen Peter Noni katika pozi  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...