Serikali
kupitia Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imezipa
Kandarasi ya thamani ya shilingi 2.9 bilioni kampuni tatu za vijana wa
Kitanzania ili kutekeleza mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu
Nyumba (Green House).
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana Mhe.Anthony Mavunde wakati akizindua mafunzo hayo Januari 05, 2019 yanayoendelea katika Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine mkoani Morogoro.
Programu hiyo ambayo itatumia jumla ya shilingi 2.9bilioni katika utekelezaji wake ambapo kampuni zilizoshinda kandarasi hiyo ni Kampuni za vijana wazalendo wa kitanzania ambao ni wabobezi katika masuala ya kilimo ikiwemo kampuni na Royal Agriculture Ltd, Holly Green Agriculture Group Ltd, na SUGECO.
Mafunzo haya yatafanyika katika Mikoa yote Tanzania Bara na kuhakikisha Halmashauri 84 zinafikiwa kwa awamu hii ya kwanza lengo likiwa ni kuwajengea vijana ujuzi kupitia kilimo cha kisasa ambapo tayari kwa mwaka huu wa fedha imeanza mafunzo hayo kwa kutumia teknolojia ya Kitalu Nyumba (Green House).
“Kwa kuanzia tutahakikisha kila Halmashauri tunatoa mafunzo kwa vijana 100 na kati yao vijana 20 watapatiwa mafunzo ya kujenga Vitalu Nyumba ili kwa wale watakaopenda kuendelea na kilimo hiki wasikose wataalamu wa kuwajengea Vitalu hivyo ”Alisisitiza Mavunde.

Mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House) na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia wenye ulemavu Mh Ikupa Stella Alex wakiangalia moja ya bidhaa wakati wa uzinduzi wa mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House).
mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House) akitembelea moja ya shamba darasa.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana **Mhe.Anthony Mavunde akizungumza katika uzinduzi wa mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House).
Moja ya Green House
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...