SHIRIKISHO la Riadhaa Duniani (IAAF) limekana kwamba litaiambia Mahakama kuwa wanariadha wote wanawake wenye viwango vikubwa vya homoni za kiume mwilini, yaani testosterone kama vile Caster Semenya wanapaswa kutambuliwa kama wanaume. Bingwa wa dunia na Olimpiki katika mbio za mita 800 anapinga sheria iliyopendekezwa na IAAF inayonuiwa kudhibiti viwango vya homoni hiyo kwa wanariadha wanawake. Kesi hiyo itasikilizwa katika mahakama ya malalamiko katika michezo (Cas) wiki ijayo.

Gazeti la the Times limeripoti kuwa mawakili wa IAAF watasema kuwa Semenya "kibayolojia ni mwanamume" pamoja na kwamba anatambuliwa kuwa mwanamke. Shirikisho hilo la riadha linasema "halitambui" mwanariadha yoyote mwenye "tofuati za kukuwa kijinsia" (DSD) ambapo raia wa Afrika kusini, Semenya ndiye anayeonekana zaidi kuwa mwanamume .

 "Kinyume na hicho, tunakubali jinsia zao kisheria pasi na shaka, na tunawaruhusu washiriki katika kitengo cha wanawake," lilisema siku ya Jumatano. "Hata hivyo, iwapo mwanariadha aliye na hali hiyo ya DSD, atakuwa na sehemu nyeti za kiume, na viwango vya kiume vya homoni hiyo ya testosterone, wanapata ongezeko la mifupa na uzito wa misuli na nguvu na huongeza damu mwilini ambayo mwanamume hupata wanapo baleghe, ndicho kinachowapatia wanaume nguvu zaidi ya wanawake katika mashindano.

"Kwahivyo, ili kuwa na ushindani wa sawa katika kitengo cha wanawake, ni muhimu kuwataka wanariadha walio na hali ya DSD kuzipunguza homoni kusalia kuwa kama za wanawake kabla hawajaruhusiwa kushiriki katika mashindano ya kimataifa" IAAF ilinuia kuuidhinihsa sheria mpya Novemba 1, 2018 lakini ikaahirisha hadi Machi 26 kusubiri matokeo ya kesi aliowasilisha Semenya na Shirikisho la Riadha Afrika Kusini. 

 Kuahirishwa huko kunamaanisha kuwa wanariadha wenye hali hiyo ya DSD hawatoruhusiwa kushiriki katika mashindano kwa miezi 6 kutoka tarehe ambayo mabadiliko ya sheria yataidhinishwa ambayo, huenda ikamfanya Semenya akakosa kushiriki baadhi ya mashindano ya msimu wa nje 2019.

Hata hivyo wakati Semenya, alipotangaza kwamba atapambana na sheria hizo mwaka jana Afrika kusini alisema: "Si haki. Nataka nikimbie kama kawaida, namna nilivyozaliwa. Mimi ni Mokgadi Caster Semenya. Mimi ni mwanamke na nina kasi." Wakati huohuo Mtafiti Mkuu Mwenza katika Chuo Kikuu cha Yale na Mtaalamu Mkuu wa masuala ya homoni hiyo ya testosterone Katrina Karkazis ni miongoni mwa walioshutumu shirikisho hilo la riadha duniani kuhusu msimamo wake. 

 Amesema IAAF "inatafasiri vibaya sayansi ya bayolojia ya jinsia" na inatafuta "kuunda ufafanuzi wake binafsi wa jinsia kutokana na imani zenye makosa kuhusu bayolojia na jinsia," na kuongeza hilo halina msingi na linaweza kuwa na madhara zaidi kwa kuidhinihsa ukosefu wa uelewa na kuchangia unyanyasaji zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...