Alhamisi ndio siku ya mwisho ya kampeni za uchaguzi nchini Nigeria, siku ya jumamosi nchi hiyo itafanya uchaguzi wa urais. Nigeria ilifanikiwa kuingia katika uongozi wa Kidemokrasia miaka minne tu iliyopita licha ya matatizo mbalimbali wanayokumbana nayo hivi sasa.

Kampeni za uchaguzi zikisindikizwa na tungo za muziki kutoka kwa waimbaji mbalimbali, Rais wa sasa na Mgombea Mohamud Buhari ameahidi kupeleka nchi hii katika hatua nyingine endapo atachaguliwa.

Buhari ndie alikua mwanasiasa wa kwanza wa upinzani kushinda uchaguzi wa nchi hiyo.Mapema wakati akifungua kampeni zake mwaka jana alisema kuwa vita ilianza muhula wa kwanza nahitaji kuendelea.

''tunawajibika kuwa kazi tuliyoanza muhula wa kwanza, ya kuhakikisha mali za nchi na rasilimali zinakua na umuhimu kwa wananchi wa kawaida'' alisema Buhari.

Lakini kuna maswali juu ya Afya ya Buhari mwenye umri wa miaka 76, amekua akisafiri mara kwa mara kwenda London kwa matibabu ya ungonjwa ambao umewekwa siri.

Kuna wagombea wengine 72 wa kiti cha urais, lakini mshindani mkuu ni Atiku Aboubakar , ikiwa ni mara yake ya nne kugombea kiti hiko.Anasifika kuwa mfanyabiashara mzuri, lakini suala la Rushwa wakati alipokua makamu wa rais linatia doa jitihada zake.

''katika uchunguzi wote uliofanywa dhidi yangu, kama mimi ni mla rushwa ama la, hakuna ushahidi uliopatikana, na kama kuna yoyote mwenye ushahidi ajitokeze, sijawahi kutuhumiwa kuhusu rushwa'' alisisitza Atiku Aboubakar.
Rais Muhammad Buhari.

KUSOMA ZAIDI BOFYA BBC Swahili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...