Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeshindwa kuendelea na usikilizwaji wa kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa sababu shahidi abdu Chemba aliyetarajiwa kutoa ushahidi wake leo, ambaye ni mfanyakazi wa clouds amepata msiba.
Wakili wa Serikali, Ashura Mzava amedai hayo leo, Februari 28, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kusikilizwa.
Amdedai katika kikao kilichopita mahakama ilimuonya shahidi huyo Abdu Chemba, na kumtaka leo kuja mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi wa shauri hilo lakini tangu juzi aliomba udhuru kwamba wanamsiba.
"Niliwasiliana na Chemba mimi mwenyewe hivyo tunaomba baada ya wiki mbili shahidi huyu aje kuendelea na usikilizaji pia tunaomba hati ya wito kwa mashahidi wengine," alidai Mzava.
Kufuatia taarifa hizo, Hakimu Simba amesema sababu zilizotolewa ni za msingi na ni udhuru ambao hauepukiki hivyo shahidi afike na wengine ili kesi iishe.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 12 mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa na wito kwa mashahidi wote ili wafike kutoa ushahidi wao umetolewa.
Mpaka sasa mashahidi watatu wa upande wa mashitaka wameshatoa ushahidi katika kesi hiyo akiwamo Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Urafiki, Mrakibu wa Polisi (SP) Batseba Kasanga.
Katika kesi ya msingi imedaiwa, Julai 3, 2017 katika ofisi za makao makuu ya Chadema zilizopo mtaa wa Ufipa wilayani Kinondoni, Mdee alitamka maneno dhidi ya Rais John Magufuli kuwa, ‘anaongea hovyo, anatakiwa afungwe breki,’ kitendo kinachodaiwa kuwa ni kumdhalilisha Rais na kusababisha uvunjifu wa amani.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeshindwa kuendelea na usikilizwaji wa kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa sababu shahidi abdu Chemba aliyetarajiwa kutoa ushahidi wake leo, ambaye ni mfanyakazi wa clouds amepata msiba.
Wakili wa Serikali, Ashura Mzava amedai hayo leo, Februari 28, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kusikilizwa.
Amdedai katika kikao kilichopita mahakama ilimuonya shahidi huyo Abdu Chemba, na kumtaka leo kuja mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi wa shauri hilo lakini tangu juzi aliomba udhuru kwamba wanamsiba.
"Niliwasiliana na Chemba mimi mwenyewe hivyo tunaomba baada ya wiki mbili shahidi huyu aje kuendelea na usikilizaji pia tunaomba hati ya wito kwa mashahidi wengine," alidai Mzava.
Kufuatia taarifa hizo, Hakimu Simba amesema sababu zilizotolewa ni za msingi na ni udhuru ambao hauepukiki hivyo shahidi afike na wengine ili kesi iishe.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 12 mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa na wito kwa mashahidi wote ili wafike kutoa ushahidi wao umetolewa.
Mpaka sasa mashahidi watatu wa upande wa mashitaka wameshatoa ushahidi katika kesi hiyo akiwamo Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Urafiki, Mrakibu wa Polisi (SP) Batseba Kasanga.
Katika kesi ya msingi imedaiwa, Julai 3, 2017 katika ofisi za makao makuu ya Chadema zilizopo mtaa wa Ufipa wilayani Kinondoni, Mdee alitamka maneno dhidi ya Rais John Magufuli kuwa, ‘anaongea hovyo, anatakiwa afungwe breki,’ kitendo kinachodaiwa kuwa ni kumdhalilisha Rais na kusababisha uvunjifu wa amani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...