Kituo cha
afya Ikwiriri Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani kinakabiliwa na changamoto ya
upungufu wa dawa ambazo hupelekwa kidogo ikilinganishwa na idadi ya wagonjwa
wanaohudumiwa katika kituo hicho huku tatizo la vifo vinavyotokana na uzazi
vikiendelea kutokea katika kituo hicho.
Mganga mkuu wa kituo cha afya Ikwiriri, Yahya Mohamed
ametoa taarifa hiyo baada ya kupokea msaada wa vifaa tiba mbalimbali ikiwemo
dawa za kusaidia kina mama wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua na vifaa
vya upasuaji kwa kina mama wanaopata uzazi pingamizi kutoka katika kikundi cha
maombi cha Our God is Good cha Jijini Dar Es Salaam.
Amesema kituo hicho kwa sasa kinahudumia idadi kubwa
ya wagonjwa hasa wasiokuwa na uwezo hivyo wakati mwingine kulazimika kutoa
huduma ya matibabu bure kwani hawawezi kumwacha mgonjwa apoteze maisha kwa
sababu tu hana fedha za kulipia
Kwa upande wake mratibu wa zoezi hilo kutoka OGG Liku
Madaki ameelezea kuwa lengo la msaada huo ni kuutaka uongozi wa kituo hicho kuitumia
kwa lengo lililokusudiwa ili kuokoa maisha ya wana Ikwiriri na Rufiji kwa
ujumla,mbali na vifaa na dawa amesema wamepeleka zawadi mbalimbali kwa ajili
ya wagonjwa:
Baadhi ya wagonjwa kituoni hapo mbali na wakishukuru kwa msaada huo,ambapo pia wameiomba serikali
kuboresha kituo hicho kwa kuhakikisha kinapata vifaa na dawa kulingana na idadi
ya wagonjwa ili kuwapunguzia umbali wa kufuata huduma ya matibabu Utete ambako
kuna hospitali ya wilaya.
Mdau wa Afya Ufoo Salo kutoka kikundi cha maombi cha Our God is Good cha Jijini Dar Es Salaam akikabidhi baiskeli ya wagonjwa kwa Mganga mkuu wa kituo cha afya Ikwiriri, Yahya Mohamed.
Mdau wa Afya Ufoo Salo kutoka kikundi cha maombi cha Our God is Good cha Jijini Dar Es Salaam akiwa amemshika mtoto walipotembelea kituo cha afya Ikwiriri, Rufiji Mkoani Pwani .

Mdau wa Afya Ufoo Salo kutoka kikundi cha maombi cha Our God is Good cha Jijini Dar Es Salaam akikabidhi baiskeli ya wagonjwa kwa Mganga mkuu wa kituo cha afya Ikwiriri, Yahya Mohamed.
Mdau wa Afya Ufoo Salo kutoka kikundi cha maombi cha Our God is Good cha Jijini Dar Es Salaam akiwa amemshika mtoto walipotembelea kituo cha afya Ikwiriri, Rufiji Mkoani Pwani .

Baadhi ya Wadau wa Maendeleo kutoka katika kikundi cha maombi cha Our God is Good cha Jijini Dar Es Salaam,wakijadiliana jambo kala ya kuanza shughuli yao ya kukabidhi msaada waoo vifaa tiba na vitu vingine kwa kituo hicho cha Afya.
Baadhi ya Wadau wa Maendeleo kutoka katika kikundi cha maombi cha Our God is Good cha Jijini Dar Es Salaam,wakikabidhi msaada waoo vifaa tiba na vitu vingine kwa Uongozi wa kituo hicho cha Afya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...