Na Ripota Wetu, Dar es Salaam.
 
Mkazi wa Keko jijini Dar es Salaam, Yusuph Julla, ameibuka na ushindi wa sh milioni 10 kutoka kwenye bahati nasibu ya biko, huku akimchagua mke wake Mwanaidi Salumu kuwa mpendanao wake kutokea kwenye vuna fedha za wapendao.

Makabidhiano hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam, kwa kuwakabidhi chao wapendanao hao wenye maskani yao Keko wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam ili waendelee na harakati zao za kimaisha.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Julla aliishukuru Biko kwa kumpatia fedha zake mapema akisema kuwa fedha hizo zitawanufaisha yeye na mkewe kwenye familia yao hiyo.

Kucheza Biko sasa ni kuanzia sh 500 na sh 1000 na kuendelea, huku ushindi wake ukianzia sh 1000 hadi sh 100000 kwa watakaocheza sh 500 hadi sh 9500 wakati  watakaocheza kwa sh 1000 na kuendelea, mchezaji anaweza kujishindia zawadi ya papo kwa hapo kuanzia sh 5000 hadi sh milioni moja bila kusahau wote kuingia kwenye droo kubwa ya Jumatano na Jumapili.

Bahati nasibu ya Biko inachezwa kwa mitandao ya simu minne ambayo ni Tigo Pesa, M-Pesa, Artel Money na HaloPesa, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba 2456, huku Watanzania wakiweza kujishindia zawadi kubwa katika droo ya Jumatano na Jumapili.
 Mshindi wa sh milioni 10 kutoka Bahati nasibu ya Biko, Yusuph Julla, akiwa na mkewe baada ya kukabidhiwa fedha zake za ushindi kutoka kwenye bahati nasibu hiyo huku Julla akimtaja mkewe Mwanaidi Salimu kuwa mpendanao wake hivyo kugawana fedha hizo kwa pamoja kwa ajili ya kufanyia mambo ya kimaendeleo. Biko inachezwa kwa njia ya ujumbe wa maandishi huku washindi wa droo kubwa wakipatikana Jumatano na Jumapili pamoja na zawadi za papo kwa hapo.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...