*Alikuwa akitokea Bukoba kwenye maziko ya Ruge Mutahaba

Na Said Mwishehe, Michuzi TV

PIGO jingine Clouds Media Group! Ndivyo unavyoweza kuzungumzia taarifa za kufariki Dunia kwa Mtangazaji wake maarufu Ephraim Kibonde.

Kwa mujibu wa taarifa za Uongozi wa Clouds Media Group kupitia kwa Sebastian Maganga ambazo wamezitoa mapema hii zinasema Kibonde amefarikia dunia leo asubuhi ya Machi 7,2019. Amesema taarifa nyingine kuhusu kifo cha Kibonde zitaendelea kutolewa ili kuufahamisha umma. 

Awali Mkuu wa Mwanza John Mongela alikuwa wa kwanza kutoa taarifa za kufariki kwa Kibonde ambapo amesema kifo chake kimetokana na kusumbuliwa na shinikizo la damu ambalo lilianza tangu akiwa mkoano Kagera.

"Ephraim Kibonde amefariki akiwa hapa mkoani Mwanza ambako alikuwa anasumbuliwa na presha tangu akiwa kwenye shughuli za mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Ruge Mutahaba," amesema Mongella.

Kibonde alikuwa miongoni kwa wafanyakazi wa Clouds Media walioambatana na waombolezaji wengine kwenda kumpumzisha kwenye nyumba yake ya milele aliyekuwa Mkurugezi wa Vipindi na Uzalishaji Ruge Mutahaba ambaye alifariki Dunia Februari 26 mwaka huu nchini Afrika Kusini.

Michuzi Media Group, ambayo ilipata kufanya mahojiano ya mwisho na marehemu Kibonde wakati wa msiba wa Ruge kupitia Michuzi TV,  inaungana na Watanzania wengine kutoa pole kwa familia ya marehemu Ephraim Kibonde,wafanyakazi wa Clouds Media Group,ndugu,jamaa na marafiki.
Bwana Ametoa,
 na Bwana Ametwaa.
Jina lake na lihimidiwe
AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...