Kampuni ya Ujenzi Zone & Mafundi Connect wameandaa Bonanza litakalowakutanisha mafundi na wadau mbalimbali wa fani ya ujenzi, bonanza litakalofanyika katika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam siku ya Jumapili March 31, 2019.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kampuni hiyo, Jacqueline Mushi amesema lengo lakuandaa bonanza hilo nikuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya Ujenzi kufahamiana, kuburudika pamoja na kuandaa mipango na mikakati kabambe ya itakayo rahisisha shughuli nzima za ujenzi. 


Mushi amesema wanakutana kutokana na wadau mbalimbali wa fani hiyo kutegemeana kwenye fani hiyo, Wazalishaji wa Vifaa vya ujenzi wanamtegemea zaidi fundi na fundi anafikisha akielewa bidhaa atafikisha ujumbe kwa wateja. 

Pia Mushi amesema wameanzisha Kampuni hiyo kwa takriban miaka Saba sasa, kutokana na changamoto mbalimbali zilizokuwa zinawakumba katika Ujenzi. Mfano uwepo wa migogoro baina ya Mafundi ya Wateja.


Moja wa Wadhamini, kutoka Kampuni ya Vifaa mbalimbali vya Ujenzi ya Import International Tanzania Limited,  Tumaini Mkojera amesema wamevutiwa na kazi za Ujenzi Zone & Mafundi Connect kutokana na Kampuni hiyo kuvutiwa na kuweka uhusiano mzuri kati ya Mafundi Ujenzi na Wateja. 


Mkojera amesema wameona ni vyema kushiriki Bonanza hilo ili kupata nafasi kukutana na Mafundi nakuwapa mafunzo yatakayowasaidia kwenye baishara zao. 

Bonanza hilo litatumia nafasi hiyo kuwakutanisha wadau hao wa fani ya ujenzi na mafundi ambapo pia litaunda Timu ya Mpira wa Miguu itakayoitwa Ujenzi FC. 
Pia litashirikisha Wasanii mbalimbali wa Bongo Fleva akiwemo Inspector Haroun 'Babu' na Banana Zoro.
Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kampuni hiyo, Jacqueline Mushi  akizungumza na waandishi wa hahari juu ya bonanza litakalowakutanisha mafundi na wadau mbalimbali wa fani ya ujenzi,  litakalofanyika katika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam siku ya Jumapili March 31, 2019.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...