Mtu mmoja ajulikanaye kwa jina la Michael John Mwandu mwenye umri wa miaka 54 mkazi wa Dumila wilaya ya Kilosa amejiua mwenyewe kwa kunywa sumu baada yakufanya mauji ya kumuua mke wake Leonola Ernest mwenye miaka 37 akiwa na ujauzito wa miezi Kati ya 7 hadi 8,

Akizungumza na waandishi wa habari Leo Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro ASCP Wilbrod Mutafungwa amewataja marehemu wengine kuwa ni mama mkwe wa muuji Magreth Yohana mwenye umri wa miaka 59,Salma Iddi jirani yao mwenye umri wa miaka 52 na pamoja yeye mwenyewe marehemu Michael John ambaye amejiua baada yakufanya mauji hayo chanzo Cha vifo hivyo ni wivu wa kimapenzi alioubaini akimtuhumu mke wake kuwa na mahusiano na mwanaume mwingine huku akidai hao wengine walikuwa wakifahamu Jambo hilo.

Marehe ametumia panga kumuua mama yake mkwe huku yeye na marehemu wengine wakinywa sumu aina ya Carbon Furan ambayo ni dawa yakuua wadudu kwenye mimea

Tukio hilo limetokea tarehe 24/5/2019 usiku huko Dumila mkoani Morogoro.
Baadhi ya waandishiwa habari wakimsikiliza Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro ASCP Wilbrod Mutafungwa wakati akizungumzia mauaji hayo.
Baadhi ya ushahidi ulioonyeshwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ACP Wilbrod Mutafungwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...