Kwa wafuasi wake sherehe hiyo ya misa ya wafu ni ushindi dhidi ya serikali iliokuwepo
Jeneza la marehemu Etienne Tshisekedi likibebwa
Rais wa Rwanda Paul kagame akitoa heshima zake za mwisho
Wale waliopata wito rasmi waliruhusiwa kuingia
Kulikuwa na biashara ya mau nje ya uwanja huo
Wafuasi wa mkongwe huyo wa upinzani walihudhuria mazishi yake
Miaka miwili baada ya kifo chake nchini Ubelgiji, mazishi ya kitaifa yamefanyika kwa kiongozi wa zamani wa upinzani nchini DR Congo Etienne Tshisekedi.
Mwili wake ulisafirishwa nyumbani siku ya Alhamisi kufuatia mgogoro kati ya familia yake na serikali ya iliopita .
Mgogoro huo ulikwisha baada ya mwanawe kuwa rais mwaka uliopita.
Makumi ya maelfu ya watu walihudhuria Ibada ya wafu katika uwanja wa mashahidi mjini Kinshasa wakiongozwa na Askofu Fridolin Ambongo.
Kanisa katoliki lenye ushawishi mkubwa nchini humo liliwataka wafuasi wake kuhudhuri kwa wingi katika mazishi hayo.
Siku ya Ijumaa , rais wa Rwanda na Angola walikua miongoni mwa idadi kubwa ya watu waliojitokeza ili kutoa heshima yao ya mwisho kwa marehemu kufuatia miaka kadhaa ya uhasama kati ya taifa lake na DR Congo.
KUSOMA ZAIDI BOFYA BBC Swahili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...