Na Ripota Wetu,Wa Michuzi TV 

MKUU wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ameapa  kupambana na wanaotorosha Dhahabu na mpaka sasa na watu wawili wametiwa Mbaroni kwa kununua dhahabu kinyume cha sheria .

Homera ameyasema hayo mkoani Katavi akiwa katika ziara ya  kutembelea  migodi mbalimbali ukiwemo wa  Dilifu ambao ni mgodi wa wachimbaji wadogo na mgodi mkubwa wa Katavi na Kapufi Mining.

Amesema  anachotaka nikuona  wachimbaji wadogo wanauza madini yao katika soko la madini lililopo mkoa huo .

Homera  ameanza majukumu ya ukuu wa mkoa ikiwa tayari  soko limeshafanya biashara kwa kununua dhahabu Gram 238, Mei 23 mwaka huu wa 2019 jambo ambalo lilimfanya aanze kufatilia na kubaini dhahabu nyingi inayopatikana mkoani Katavi inauzwa nje ya mkoa hali iliyonayosababisha soko hilo kusua sua.

Amesema  kutokana na hali hiyo bosi huyo wa mkoa alimua kufanya ziara ambayo ilikwenda kuyafanyia kazi mapungufu ya soko hilo ambapo hadi  sasa linaridhisha na kufuatia oparesheni mbalimbali zinazoendelea Soko linaendelea  kufanyika kwa ununuzi na uuzaji wa madini na mpaka sasa Grams 6317.2 sawa na Kg 6 na Grams 317.2 yenye thamani ya Sh. 519,155,127.56 zimenunuliwa kwa kipindi cha Mei na Juni 30/2019 na Serikali kupata mrahaba (Royality7%) Sh. 36,340,858.92 na Service levy asilimia 0.3  sawa na Sh.1,401,718.85,

Pia  amefafanua kuwa  ameimarisha mifumo ya Benk mbili katika soko hilo nakwamba  ameendelea kuwa bana mablokers na wanunuzi wenye leseni na wachimbaji mbalimbali  kuhakikisha pia wanauza madini yao kwenye soko la mkoa ili kujenga  uchumi wa Tanzania na kumuunga mkono Rais Dk.John Magufuli katika kuinua uchumi na miundombinu ya nchi  kwa kulipa kodi.
 Wachimbaji wadogo wadogo wakimsikiliza  MKUU wa Mkoa wa Katavi Juma Homera  akiwa katika ziara ya  kutembelea  migodi mbalimbali ukiwemo wa  Dilifu ambao ni mgodi wa wachimbaji wadogo na mgodi mkubwa wa Katavi na Kapufi Mining.
 

 MKUU wa Mkoa wa Katavi Juma Homera  akiwa katia ziara ya  kutembelea  migodi mbalimbali ukiwemo wa  Dilifu ambao ni mgodi wa wachimbaji wadogo na mgodi mkubwa wa Katavi na Kapufi Mining.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...