Tanzania kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano wa 53 wa Utoaji wa Utabiri wa Hali ya Hewa wa Msimu wa Mvua za Vuli 2019 “Fifty Third Greater Horn of Africa Climate Outlook Forum” (GHACOF 53) utakao fanyika katika  Hotel ya Kilimanjaro (Hyatt Regency) kuanzia tarehe 26 hadi 28 Agosti 2019 Dar es Salaam.

Lengo la mkutano huo ni kujadili na kuandaa kwa pamoja utabiri wa msimu wa mvua za vuli za mwezi Oktoba hadi Desemba 2019, pamoja na kuandaa mikakati ya kukubaliana na hali mbaya ya hewa kwa msimu huo kwa kulenga sekta muhimu za kijamii na kiuchumi ambazo ni pamoja na afya, kilimo na usalama wa chakula, maji, nishati n.k.

Mkutano huo utajumuisha nchi za Pembe ya Afrika ambazo ni Tanzania, Kenya, Somalia, Ethiopia, Sudan, Sudan ya Kusini, Uganda, Burundi, Rwanda, Djibouti na Eritrea

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...