Kaimu Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Dkt. Kiagho Kilonzo akizungumza na waandishi habari katika maonesho ya Tamasha la Utamduni wa Juimuiya ya Afrika Mashariki (Jamafest)linalofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 

Kaimu Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Nchini  Dkt.Kiagho Kilonzo ameutaka umma wa watanzania kutembelea bodi ya Filamu katika tamasha la Utamaduni wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  (Jamafest) katika kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na bodi hiyo.

Kaimu Katibu Mtendaji Dkt.Kilonzo ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi habari katika maonesho hayo na kuwaasa watanzania kutumia chombo hicho katika kukuza sanaa ya filamu nchini kwa kuleta maendeleo.

Amesema kuwa katika maonesho hayo wataona vitu mbalimbali ambavyo vimefanywa na watanzania  kwa kutengeneza filamu ambazo zina maadili na pale ambapo wanaona filamu zilizozalishwa hazina maadili wanachukua hatua kuhakikisha hazionyeshwi.

Dkt. Kilonzo amesema kuwa maonesho hayo ni fursa kwa Tanzania na kuona namna ya nchi wanachama wengine  wanavyofanya utamduni wao  huku  wakijifunza utamduni wetu.

"Natarajia wataopita katika banda la bodi ya filamu watajifunza vitu vingi ambavyo vitawasaidia kuingia katika sekta ya filamu na kuweza kuzalisha ajira zao pamoja na taifa kupata maendeleo katika sekta hiyo"amesema Dkt. Kilonzo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...