Mdau wa michezo mkoani Iringa Mess Chengula akiwasalimia wachezawa timu mbili zilizokuwa zimeingia fainali ya mashindano ya UVCCM CUP Kata ya Mkwawa yaliyofanyikia katika chuo cha mkwawa mkoani Iringa
Mdau wa michezo mkoani Iringa Mess Chengula akimkabidhi kapteni wa timu ya Donbosco fc ambayo imeibuka bingwa wa mashindano ya UVCCM CUP Kata ya Mkwawa kwa ushindi wa penat 5-3 dhidi ya Don south baada ya sare ya 1-1 katika uwanja wa chuo cha Mkwawa kwa kijinyakulia ng’ombe mmoja.
Mdau wa michezo mkoani Iringa Mess Chengula akiwa na wadau na viongozi wa CCM kata ya mkwawa wakifauatilia fainali ya mashindanohayo.
Mdau wa michezo mkoani Iringa Mess Chengula akimkabidhi kapteni wa timu ya Don south ambao waliibuka kuwa washindi wa pili.

NA FREDY MGUNDA, IRINGA
VIJANA manispaa ya Iringa wametakiwa kuzingatia nidhamu na juhudi katika mazoezi kwa lengo la kufikia mafanikio katika michezo na kukuza zaidi vipaji walivyojaliwa na mwenyezi mungu.

Hayo yamesemwa na mdau wa michezo mkoani Iringa Mess Chengula wakati wa fainali ya mashindano ya UVCCM CUP Kata ya Mkwawa,iliyofanika katika uwanja wa chuo kikuu cha Mkwawa na kuhudhuliwa na wapenzi wengi wa mpira wa miguu mkoani Iringa.

Chengula alisemakuwa Mkoa wa Iringa umebarikiwa na vipaji vingi vya mpira wa miguu kwa kuwa amefanikiwa kuwaona vijana wengi waliokuwawanacheza fainali ya mashindano ya UVCCM CUP Kata ya Mkwawa na ameahidi kuhakikisha ataendelea kusaidia michezo ndani ya mkoa wa Iringa.

“Nimefarijika sana baada ya kuona vijana walivyokuwa na vipaji vya kusakata kabumbu maana nimebarikiwa kwa kuwaonakwamacho yangu vijina walivyokuwa wamechangamka kusakata soka uwanjani hapa chuo cha Mkwawa” alisema Chengula

Chengula amewataka wadau mbalimbali kuandaa mnashindano mbalimbali ambayo yanakuwa yanawakusanya vijana wapenda michezo na kuwawekasehemumojaambayo inakuwa inabarisha mtazamo kwenye akili za watu ambao wanakuwa wanahudhuria michezo hiyo.

“Kwanza nimpongeze diwani wa kata ya Mkwawapamojana viongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) kwa kuwaunganisha vijana pamoja na kuwaweza kuwa na lugha moja ya kimichezo na kuweza kubarishana mawazo ya kimaendeleo walipokuwa viwanjani” alisema Chengula

Aidha Chengula alisema kuwa michezo inaleta chachu kwa vijana kwenda kumchagua kiongozi wanayemtaka katika serikali za mitaa ambazo hivi karibuni utafanyika nchi nzina hivyo zoezi la kuwakusanya vijana pamoja linaleta picha nzuri ya uchaguzi.

“Rais wa Dr John Pombe Magufuli amewafundisha uzalendo wa kufanya kazi nakujitegemea na kufanya kazi kwa uhuru na ndivyo wananchi wote tunatakiwa kufanya kazi kwa kujituma na kujitafutia mali zetu wenyewe” alisema Chengula

Naye Mdhamini wa Mashindano Amiri Zakaria Kalinga ambaye ndiye diwani wa kata ya Mkwawa alisema kuwa lengo la mashindano hayo ni kuwaunganisha vijana kuwa wamoja na kutambua kuwa michezo ni ajira namichezoinaimarisha kuwa na afya njema.

“mashindano ya UVCCM CUP Kata ya Mkwawa yameshirikisha timu za kata ya mkwawa kwa kuendeleza kuwaunganisha kuwa wamoja kamaambaovyotupo hivi sasa” alisema Kalinga

Kalinga alisemakuwakata ya Mkwawa ina viwanja vingi ambavyo sio bora kama viwanja vya chuo kikuu kwa ubora hivyo tunatakiwa kutafuta wadau kuhakikisha tunatengeneza viwanja vyetu wenyewe.

Na katika fainali hiyo Timu ya Donbosco fc imeibuka bingwa wa mashindano ya UVCCM CUP Kata ya Mkwawa kwa ushindi wa penat 5-3 dhidi ya Don south baada ya sare ya 1-1 katika uwanja wa chuo cha Mkwawa kwa kijinyakulia ng’ombe mmoja.

Huku mshindi wa pili Don south na Mshindi wa tatu Dream team kutoka ikonongo kwa penati 5-4 baada ya sare tasa dhidi ya hoho fc ya itamba wote walipata mbuzi moja moja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...