Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Sanlam kitengo cha bima ya maisha, Khamis Suleiman (Kushoto), akizungumza na waandishi wa habari katika hafla fupi ya kuwazawadia washindi wa mashindano yalioisha hivi karibuni yaitwayo “Life is a Marathon competition” na
kuwapa fursa ya kwenda kushiriki na kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya fainali ya “Sanlam Cape Town Marathon”, katika ofisi za makao makuu ya kampuni hiyo, jiji Dar es Salaam, jana. Kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Sanlam kitengo cha bima Gift Noko.


=========   ========  ======

Kampuni ya Sanlam Tanzania imetoa zawadi kwa washindi wa mashindano yalioisha hivi karibuni yaitwayo “Life is a Marathon competition” na kuwapa fursa ya kwenda kushiriki na kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya fainali ya “Sanlam Cape Town Marathon” yatakayo fanyika tarehe 15 septemba mwaka huu. 

Washindi hao ni Jamia Abdallah na lister Lusulo Pakua. Vile Vile balozi wa Sanalam Maulid Kitenge na wateja wa Sanlam Stephen Mndeme na Innocent Shaku wamepata nafasi ya kushiriki katika mashindano hayo. 

Hatua ya kwanza ya mashindano ya “Life is a Marathon competition” yalihusisha washindani kuwasilisha picha na video zao zikionyesha jinsi watakavyo jiandaa kushiriki katika mashindano hayo, baada ya hapo washindi walichaguliwa na kupitia mazoezi mbali mbali ya kujiandaa. 

Akizungumza katika hafla ilyofanyika ofisi za Sanlam Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Mr Khamis Suleiman, aliwapongeza wachezaji kwa kujituma kwao na kuwasihi kuonyesha juhudi zaidi katika mashindano yanayokuja. 

“Tunafuraha sana kuona jinsi wachezaji hawa walivyofanya vizuri na mkiwa mnajianda kusafiri napenda kuwatia moyo mkafanye vizuri zaidi. Iwe unafanya mazoezi kwa ajili ya mashindano ya mbio au unajifunza kuendesha baiskeIi inabidi uwe na mshirika ambaye atakusaidia kufanikisha malengo yako, na hii ndio ngao yetu hapa Sanlam Tanzania, tumejikita katika kutuoa huduma na bidhaa za kidigitali ambazo zitakusaidia wewe katika hatua zote za maisha.” 

Sanlam ilizindua mashindano ya “Life marathon” tarehe 8 Agosti kwa lengo la kuonyesha umuhimu wa ushirikiano katika kuwezesha watu kufanikisha malengo yao na kuwa na maisha bora, pia ni moja ya njia ya kampuni ya Sanlam kutambua na kuwapongeza wanamichezo mbali mbali nchini Tanzania 

Ikiwa ni mashindano pekee ya marathon yenye daraja la dhahabu barani Africa, Sanlam Cape town marathon huleta pamoja zaidi ya vilabu 23 vya kimataifa na wakimbiaji takribani 15,000 kila mwaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...