NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA

WAZAZI, walezi mkoani Pwani, wametakiwa kumpa hazina ya elimu mtoto na kumwekezea elimu ikiwa ni urithi mkubwa wa maisha yake ,badala ya kumpatia vitu vya kifahari kama magari suala ambalo linachangia kurudisha nyuma maendeleo yake kitaaluma .

Aidha watoto wameaswa kuacha kujiingiza katika tabia hatarishi kama vile kutumia madawa ya kulevya ikiwemo bangi na badala yake wawe na hofu ya mungu kwa kufuata maadili mema.

Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo alitoa rai hiyo wakati wa mahafali ya 14 ,ya  darasa la saba ya shule ya msingi Kibaha Independent (KIPS )iliyopo Kibaha.

Aliwataka wazazi na walezi wenyewe kumtengeneza mtoto kwa kumuandaa  na kesho yake kwa kumfuatilia muenendo wa masomo yake .

"Muda wa kuwapa magari na simu kubwa za kiganjani utafika , ,Tuwawezeee elimu kwa manufaa yao baadae":-Wanangu safari yenu bado mbichi, elimu ni bahari ,pambaneni ,Tanzania inasubiri vijana wasomi ,msiwe na haraka na mambo ya dunia na ya ovyo ovyo kwani maisha hayataki haraka"alisisitiza Ndikilo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa wakurugenzi wa NJUWENI na bodi ya shule hiyo, alhaj Yusuph Mfinanga alisema, ili kuepukana na utapeli kwa malipo mbalimbali shuleni hapo wazazi wanapaswa kulipa ada na michango kupitia akaunti ya shule badala ya kukabidhi fedha mkononi .
Awali mkurugenzi wa shule hiyo ,Nuru Mfinanga alieleza, kwa sasa wanafanya upanuzi wa kwa kujenga shule eneo la Mwanalugali ili wanafunzi wanaojiunga shuleni hapo wasikose nafasi kutokana na ufinyu wa eneo la sasa na kuongoza mikondo.

Nuru alibainisha ,wanafunzi wanafanya vizuri kitaaluma kwani mwaka 2016 shule hiyo ilikuwa ya 16 kati ya shule 323, mwaka 2017 ilikuwa ya nne na mwaka 2018 ilikuwa ya nne hivyo mwaka huu wanatarajia kufanya vizuri zaidi .
Jumla ya wahitimu 82 walitunukiwa vyeti vya kuhitimu elimu ya msingi kwa mwaka 2019 shule ya msingi KIPS.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...