Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Serikali imesema kuwa vyazo vya maji vinatakiwa kulindwa kwa wenye viwanda wanatakiwa kulipa tozo zilizoaininishwa kisheria kutokana na wenye viwanda kutumia kiasi kikubwa cha maji.

Hayo ameyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo wakati alipokutana na wenye viwanda katika Ofisi ya Bonde la Wami/Ruvu  jijini Dar es Salaam, amesema kuwa watamshauri Waziri Mwenye dhamana kuwa kuwepo kwa tozo moja kwa wenye viwanda nchini kulipa katika mabonde.

Amesema kuwa mabonde Tisa nchini ndio wana mamlaka ya kuchukua tozo wa ajili ya kuhifadhi maji kwani kuwepo kwa hayo maji inatokana na mabonde hayo kulinda vyanzo vya maji.

“Mabonde haya yanahitaji kugharamia vyazo kwa maji hivyo wenye viwanda wasipolipa shughuli za mabonde hazitafanywa katika ufanisi wa kulinda maji hayo wanayoyatumia katika uendeshaji wa viwanda vyao”amesema Profesa Kitila Mkumbo.

Amesema kuwa mahitaji ya maji ni ya kila siku na kuna watu wanafanya kazi ya kuangalia katika vyazo vyake na kisha watu kuyatumia kutokana na kusimamiwa na hayo mabonde.

Nae Mwakilishi wa Wamiliki wa Wenye Viwanda nchini (CTI) Hussein Sufiani amesema kama wenye viwanda wamekubali kulipa tozo na ada.
 Katibu wa Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya mazungumzo na wamiliki wa Wenye Viwanda (CTI) kuhusiana na ulipaji wa tozo za maji katika mabonde katika mkutano ulifanyika katika ofisi za Bonde la Wami/Ruvu jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi  wamiliki wa Wenye Viwanda (CTI) Hussein Sufiani akizungumza kuhusiana na majadiliano kwa wenye viwanda katika ulipaji wa tozo na ada katika mkutano ulifanyika katika ofisi za Bonde la Wami/Ruvu jijini Dar es Salaam. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...