MKUU wa Wilaya ya Ikungi
mkoani Singida, Edward Mpogolo amewata wananchi wa Wilaya hiyo kutumia
muda uliobaki kujiandikisha katika daftari la uchaguzi wa serikali za
mitaa ili waweze kutumia haki yao kuchagua viongozi.
Mpogolo
alisema hayo leo alipozungumza na waandishi wa habari katika Kitongoji
cha Mtakuja, Kijiji cha Ikungi katika Wilaya hiyo alipokwenda
kujiandikisha, aliwataka wananchi wa Ikungi kutumia haki yao ya
Kidemokrasia ya kuchagua na kuchakuliwa.
Aidha
amesema uchaguzi ngazi wa serikali ngazi ya Vitongoji na Vijiji ni
muhimu wananchi hushiriki moja kwa moja kupanga na kuamua kutekeleza
maendeleo yao.
"Hivyo
ni muhimu kwa kila mwana Ikungi kushiriki kwakuwa inaamua hatima yake
ya kujiletea maendeleo ambayo Rais John Magufuli amekuwa akipambana kwa
watanzania.
Alisema
hadi jana wameandikikura.zaidi ya asilimia 41 ambapo wameweka mikakati
kuhakikisha wanafikia lengo la kuandikisha watu 154137.
Mpogolo
aliwahimiza wananchi aliowakuta katika kituo hicho pamoja na vituo
vingine alivyotembelea kuwahimiza vijana wao ambao umri wao ni juu ya
miaka 18 kuhakikisha nao wanajiandikisha ili waweze kupata nafasi ya
kuchagua viongozi ambao watawaletea maendeleo.
"Wazee
wangu, tuwahimize na vijana wetu nyumbani nao wajiandikishe tusikubali
wakabaki bila kujiandikisha nafasi hii ni muhimu kuitumia ili nao wawe
sehemu ya kuchagua viongozi wanaowataka," alisema Mpogolo.
Aidha,
alisema maendeleo katika nchi hayawezi kushuka kutoka Mbinguni bali kwa
kuchagua viongozi imara, wenye mapenzi na maendeleo ya wananchi na pia
maendeleo ya nchi yao.
Mpogolo
alitembelea vituo vingine katika Wilaya hiyo ambapo alizungumza na
wananchi kujua changamoto zao katika uandikishaji huo na pia
kuwahamasisha kuwashauri na watu wengine kujitokeza.
"Msiwaache watu nyumbani tuhakikishe wote wanajiandikisha, kina mama nyumbani, majirani," alisema.
Mpogolo
alisema katika Wilaya hiyo uandikishaji unaenda vizuri, watu
wanajitahidi kujitokeza na pia viongozi wanajitahidi kuhamasisha
wananchi kujitokeza ili kuhakikisha kila mmoja anashiriki kupiga kura.
MKUU wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Edward Mpogolo akijiandikisha katika daftari la uchaguzi wa serikali za mitaa,katika Kitongoji cha Mtakuja, Kijiji cha Ikungi Wilayani humo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...