

Mwezeshaji kutoka Shirika la Amani Girls Home Bw. Mang’olo Shoma Bahati akieleze jinsi Mradi wa Vijana Maisha ni Kazi unaotekelezwa na Shirika la Plan International ulivyowasaidia vijana wa Kikundi cha Shilabela cha Buhongwa wakati Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ilipokuwa inatembelea Mashirika yaliyopo Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika Mashirika.

Afisa Miradi kutoka Shirika la Plan International Bw. Nicodemas Gachu akielezea kuhusu utekelezaji wa Miradi inayotekelezwa na Shirika hilo wakati Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ilipotembelea Miradi inayotekelezwa na Shirika hilo mkoani Mwanza katika ufuatiliaji wa mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika Mashirika hayo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Dkt. Richard Faustine Sambaiga (Mwenye koti) akikabidhi mchango wa jamii kwa mmoja wa mjumbe wa kikundi cha Shilabela kilichopo Buhongwa jijini Mwanza wakati Bodi hiyo ilipokuwa inatembelea Mashirika yaliyopo Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika Mashirika hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...