Kuelekea siku ya Vyoo Duniani wadau mbalimbali wa Afya nchini wametakiwa kutambua changamoto zinazowakabili watu ambao wanajihusisha na uzibuaji wa mitalo mikubwa pamoja na kutapisha mashimo ya Vyoo.


Imeelezwa kuwa katika jiji la Dar es Salaam zaidi ya asimilia 70 ya wakazi wake yapo katika maeneo ambayo si rasmi. Maeneo hayo sifa zake kunakuwa na changamoto za upatikanaji wa maji safi na Salama, upatikanaji wa huduma za usafi pamoja na huduma za utupaji wa taka maji.


Hayo yamebainishwa na Meneja miradi mwandamizi wa Taasisi ya WATER AID Tanzania, Bw.Twaha Mubarak  alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wake na Waandishi wa habari kwenye ofisi za taasisi hiyo ya WATER AID jijini Dar es Salaam.


Akizungumza na wanahabari Bw. Twaha amesema kuwa inakadiliwa asilimia 10 ya jiji la Dar es Salaam limeunganishwa katika mfumo wa maji taka hivyo kunakuwa na uwezekano mkubwa wa kuibuka magonjwa mbalimbali yanayoambukiza.


"Tukizungumzia katika asilimia hizo, asilimia 90 zilizobaki tunatumia aina nyingine za mifumo, moja kwa moja tunatakiwa kufahamu wanaofanya kazi hizo (kutapisha vyoo) ni wale ambao wanaitwa majina mengi kama vyura ama wavamiaji lulu". Amesema Bw. Twaha.

Aidha Bw. Twaha amesema kuwa katika ripoti ambayo imeandaliwa imezungumzia changamoto hizo kwa mfanya usafi na imesheheni na kudadavua mkanganyiko wanaopitia wafanyakazi katika sekta ya usafi kwenye nchi zinazoendelea.

Twaha amesema kuwa ripoti hiyo  imeandikwa kwa pamoja kwa shirika la kazi Umimwwnguni, Shirika la Water Aid, Benki kuu ya Dunia na Shirika la Afya Duniani, lengo hasa ni kuinua ufahamu  kuhusu Mazingira hatarishi ambayo wafanyakazi hao wanayapitia.

Amesema Wafanyakazi hao mara nyingi hugusa kinyesi cha binadamu pasipokuwa na vifaa vya kujikinga wala vitendea kazi vilivyobora, kitu ambacho kinawaweka kwenye hatari za kupata magonjwa mbalimbali.

Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Mazingira na Watu (UMAWA) inayofanya biashara ya usafi wa mazingira katika upakuaj wa vyoo na uchakatishaji wa maji taka, Bw.Mathias Milinga amesema kuwa biashara hiyo imekuwa kwa kiasi tangu kuanzishwa kwake kwani mpaka sasa katika maeneo mengi hasa wilayani Kigamboni upakuaji holela wa vyoo umepungua kwa kiasi kikubwa.

"Wapakuaji wa kienyeji wakipata kazi mara nyingi wanakuja kwenye kituo, tumefauru kupanua huduma hiyo kwa kufanya matangazo katika vipeperushi lakini pia tunafanya kazi na halmashauri hasa kamati za afya". Amesema Bw.Milinga.
 Meneja Miradi Mwandamizi wa Taasisi ya WATER AID Tanzania, Bw.Twaha Mubarak akizungumza na wanahabari katika ofisi za taasisi hiyo  jana jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mazingira na Watu (UMAWA) inayofanya biashara ya usafi wa mazingira na uchakatishaji wa maji taka, Bw.Mathias Milinga akizungumza na wanahabari katika ofisi za taasisi ya WATER AID jana  jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...