Madarasa yaliyoezuliwa na mvua shule ya msingi Namindondi.
Shule ya Namindondi iliyopo Wilaya ya Tandahimba imeezuliwa paa na mvua wakati wanafunzi wa darasa la nne wakifanya Mtihani wa Taifa

Akizungumza na kutoa maelekezo katika eneo la tukio,
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tandahimba Said Msomoka amesema kuwa tayari hatua za utekelezaji zimechukuliwa ili kuhakikisha Wanafunzi wanaendelea na masomo

"Tunashukuru hakuna mwanafunzi aliyeumia na wanafunzi waliendelea na mitihani kwa kuhamishiwa darasa lingine,kwa hiyo utekelezaji utaanza rasmi kesho ili  hadi kufikia  jumatatu wanafunzi waendelee na masomo,"alisema Msomoka

Naye Kaimu Mkuu wa shule Juma Kasidi alisema mvua hiyo ilikuwa yenye upepo mkali iliyoambatana na radi  ilisababisha uharibifu  wa madarasa matatu likiwemo  darasa la nne ambalo walifanyia Mtihani wa Taifa


"Ilikuwa muda wa mchana wakati darasa la nne wanamalizia Mtihani wa Taifa, somo la maarifa ya jamii ndipo tukio hilo lilitokea na hivyo tuliwahamishia wanafunzi darasa lingine wakaendelea na  mitihani,hakuna aliyejeruhiwa,"alisema Kasidi
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tandahimba Said Msomoka akitoa maelekezo kwa Mwenyekiti wa bodi ya shule

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...