Na.Khadija seif, Michuzi TV

KAMPUNI ya kusamabaza filamu nchini  Steps Entertainment imeahidi kuziba pengo lililoachwa kwa muda mrefu katika soko la filamu.

Akizungumza hayo wakati wa uzinduzi wa mfumo wa DVD wa filamu ya kashinde Meneja kutoka Kampuni hiyo Kambarage Ignatius amesema wasanii na wadau wa filamu walikua wanapata tabu kusambaza kazi zao lakini kwa Sasa muafaka umepatikana .

"Hapo awali Kampuni ya steps ilikua ikisambaza kazi za filamu lakini kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo ilibidi isimame kwa muda ili kurekebisha baadhi ya vitu,"

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya kutengeneza filamu (LUGWA COMPANY) Luckyness mokiwa amesema ni wakati wa wadau, wasanii na waandaaji wa filamu kujinua upya kutokana na kurudi kwa wasambazaji hao .

"Ni kishindo kikubwa ambacho wamefanya Kampuni ya steps na wameanza na kusambaza kazi yangu mpya ya filamu ya kashinde ambayo nilizindua mwaka huu,"

Hata hivyo Mokiwa amesema anatarajia kufanya uuzaji wa mfumo wa DVD wa filamu ya kashinde desemba 29 mwaka huu katika ukumbi wa uliopo kibaha.

Ndani ya filamu hiyo wapo wasanii kama gabo,patcho Mwamba,frola Mvungi,husna sajenti na wengine wengi huku maudhui ya filamu hiyo ikimuelezea msichana kashinde ambae ni kondakta wa daladala ambae anafanya jitihada zote ili aweze kujikwamua kimaisha.

"Lengo la kuuza filamu hiyo kibaha ni kutokana na sehemu nyingi za mandhari katika filamu hiyo imefanyika kibaha hivyo tumeona sio vibaya tukafanya shughuli ya kuuza filamu hiyo huko huko ili kuonyesha kuwa wapenzi na wadau wasanaa pia wanapatikana sehemu mbalimbali sio Dar es salaam peke yake tu japo ndio jiji la starehe,"
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lugwa Luckyness Mokiwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uuzwaji wa filamu ya kashinde kwa mfumo wa DVD ambapo Kampuni ya usambazaji wa kazi za filamu (steps entertainment) itakua ndio kazi ya kwanza kusambaza baada ya kurudi kwa kishindo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...