Timu ya Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Fuwai Hospital  wa nchini China wanatarajiwa kuwasili nchini Tanzania Novemba 28-30,2019. 

Timu hiyo ya Madaktari Bingwa itaungana na Madaktari wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kufanya upasuaji kwa wagonjwa, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mkataba wa Ushirikiano uliosainiwa wakati wa ziara ya Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu nchini China iliyofanyika mwezi Agosti 2019. 

Hospitali ya Moyo ya Fuwai inaongoza ulimwenguni katika taasisi za matibabu ya Moyo ikiwa na vitanda 1200. Kupitia ushirikiano wa hospitali hiyo na JKCI- wataalam mabingwa wa Moyo kutoka JKCI wameanza kupata mafunzo katika hospitali ya FUWAI yanayojumuisha mafunzo ya teknolojia iliyovumbuliwa na Daktari Bingwa Prof PAN ijulikanayo kama (Percutaneous And Non-fluoroscopical procedure) ambayo imepunguza kwa kiasi kikubwa gharama za upasuaji wa moyo. Habari Picha kwa hisani ya Mdau Phelisters Wegesa-Beijing China.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...