Na Woinde Shizza Michuzi Tv, ARUSHA

WAMILIKI saba wa viwanja katika eneo la Naura jijini Arusha, wamemuomba Rais John Magufuli, kuingilia kati mgogoro kati yao na Halmashauri ya Jiji la Arusha uliodumu kwa kipindi cha zaidi ya miaka 32.

Wakizungumza leo  Novemba 21,2019, wamiliki wa viwanja hivyo, wakiongozwa na Issack Kassam,Manleo Auye,Joshua Kaiza Ndosi, Kanubhai Rameshner Patel na Akber H.Sanjani, wamesema viwanja hivyo wanamiliki kwa mujibu wa sheria na wana hatimiliki.

 “Tunamuomba Rais Magufuli atusaidie tupate haki yetu tuliyoitafuta kwa muda mrefu kwani tumepita katika ofisi mbalimbali za umma tumekuwa tukizungushwa bila ya kupata msahada wowote,”amesema Sanjani.

 “Rais wetu ni kiongozi anayejali watu hususani wanyonge sisi tunaamini suala letu atalifanyia kazi hatujawahi kuwa na mashaka na utendaji kazi wake,”alisema Ndosi.

 Kwa mujibu wa nyaraka za umiliki wa eneo hilo, zinaonyesha kwamba halmashauri ya Jiji la Arusha iliwagawia maeneo hayo kwa wananchi, kati ya mwaka 1986/1987  .

Kwa mujibu wa maelezo ya wamiliki wa viwanja hivyo, walisema  baada ya kupewa maeneo hayo waliomba vibali vya kujenga na kuendeleza maeneo hayo.

Kwa mujibu wa nyaraka za siri kutoka kwa wamiliki wa eneo hilo, kwenda Halmashauri ya Jiji la Arusha inaonesha Julai 25 ,2019, walituma maombi ya kupewa vibali vya kujenga ukuta katika kiwanja namba 17,kitalu “U”sehemu F.

“Sisi wamiliki halali wa kiwanja tajwa hapo juu chenye namba 10258, ni muda mrefu sasa hatujaendeleza viwanja hivi kulingalina na mgogoro uliopo katika eneo hilo, hata hivyo tumekuwa tukilipa kodi ya serikali hadi leo,”

“Kwa barua hii tunaleta ombi kwako la kuomba kibali cha ujenzi wa ukuta kuzunguka eneo letu ili tuweze kuendelea na mipango iliyopo katika kiwanja bila ya kusumbuliwa,”imesema sehemu ya barua.

Aidha walisema baada ya mgogoro huo kudumu kwa muda mrefu mwaka 1996, walipokea barua ya kurejeshewa viwanja hivyo. Mwaka 1999, Wizara ya Ardhi kipindi hicho,ilitoa agizo kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mkurugenzi wa halmashauri na Meya wa Jiji la Arusha kurudisha maeneo hayo kwa mahusika ili wayaendeleze.
 
“Viwanja hivi tuna hatimiliki  kwa vipindi vyote tumeomba vibali vya kuviendeleza nakujenga lakini hatukupewa kilichotokea ofisi zote za serikali tulizopita kudai haki yetu wametuzungusha bila ya kutupa masahada wowote,”aliongeza 

Kwa mujibu wa hatimiliki  hiyo, inaonyesha kuwa wamiliki wa maeneo hayo, wameshailipa halmashauri ya Jiji la Arusha kodi hadi kufikia mwaka 2020.

“Chakushangaza maeneo yetu yamekodishwa kwa kampuni moja ya ujenzi kutoka nchini China bila ya sisi kujulishwa wakati tunamiliki kisheria,”alisema.

 “Taarifa tulizonazo ni kwamba kampuni hii ya ujenzi inalipa kodi kiasi cha sh.milioni 50, kwa mwezi tunataka kufahamu ni nani aliyekodisha eneo letu pia anayopokea kodi  wakati wahusika tupo ,”alisema 

Kwa mujibu wa nyaraka hizo, zinaonyesha Issack Kassam anamiliki ploti namba 19, bloku “U”,eneo F, Manleo Auye ploti namba 16, bloku “U”eneo F, Joshua Kaiza Ndosi ploti namba 21, bloku “U”eneo F, Kanubhai Rameshner Patel ploti namba 22, bloku “U” eneo F.
Muonekano wa eneo la viwanja lenye mgogoro kati ya wamiliki ma Halmashauri ya Jiji la Arusha, na viwanja hivyo vimekodishwa kwa kampuni ya ujenzi kutoka China

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...