*Spika Ndugai azishauri ofisi za Balozi kutoa ushirikiano wa kutosha
Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
SERIKALI
ya China kupitia Ubalozi wake hapa nchini umeingia makubaliano na asasi
saba za kiraia; huku mlengo mkubwa wa makubaliano hayo ukiwa ni
kushirikiana na wanajamii ikiwa ni pamoja na kubadilisha uzoefu na
teknolojia ili kuweza kujenga uchumi imara kwa wanajamii pamoja na
kupunguza umaskini.
Akizungumza
katika hafla hiyo mgeni wa heshima na Spika ya Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai amesema kuwa, viongozi wa asasi
hizo zisizo za Kiserikali kutoka Tanzania na China watashirikiana katika
kuleta maendeleo kupitia nyanja mbalimbali ikiwemo kubadilishana uzoefu
na teknolojia sambamba na kuwashirikisha wananchi katika fursa
mbalimbali za kiuchumi.
Spika
Ndugai amesema kuwa mpango huo ni wa muda mrefu ambao Rais wa nchi hiyo
Xi Jinping aliuanza mwaka 2003, Rais Jinping alianzisha ushirikiano huo
ili kuleta maendeleo ya pamoja na hiyo ikiwa sambamba na uimarishaji wa
miundombinu, biashara ya pamoja na mahusiano bora ya wanajamii.
Amesema kuwa Tanzania na China wamekuwa ndugu Sasa kutokana na kuwa na urafiki na ushirikiano uliobora zaidi;
"Tanzania
ina marafiki wengi, ila urafiki wetu na China umekuwa urafiki wa pekee,
uliodumu kwa muda mrefu na tumekuwa tukishirikiana kwa mambo mengi
yenye tija katika mataifa yetu" ameeleza Ndugai.
Ndugai
amezishauri ofisi za Balozi za mataifa hayo mawili kutoa ushirikiano wa
kutosha ili malengo ya yaliyowekwa ikiwemo kupunguza umaskini,
kubadilishana uzoefu hasa teknolojia na kutoa fursa kwa wananchi
kushiriki katika shughuli za kiuchumi kupitia asasi za kiraia yalete
mafanikio makubwa.
Kwa
upande wake Naibu Spika wa Bunge la Jumuiya wa watu wa China na kiongozi
mkubwa wa Chama cha Communist nchini humo Ji Bingxuan amesema kuwa
mahusiano hayo ambayo yana zaidi ya miaka 50 sasa yalijengwa na waasisi
wa mataifa hayo na matunda ya misingi hiyo yanashuhudiwa sasa.
Spika
Bingxuan amesema kuwa uhusiano wa Tanzania na China ni wa kipekee huku
akitolea mfano kwa Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim kuwa
kiongozi wa kwanza kutoka bara la Afrika kutunukiwa tuzo heshima ya kuwa
na kuimarisha mahusiano baina ya mataifa hayo nchini.
Vilevile
Balozi wa China nchini Wang Ke amesema kuwa fursa hizo zitawanufaisha
wanajamii wa nchi hizo kupitia asasi hizo za kiraia na kuleta maendeleo
ya pamoja.
Wang Ke
amesema kuwa mwaka 2013 Rais Xi Jinping aliichagua Tanzania kuwa nchi ya
kwanza kuitembelea mara tu alipochaguliwa na kadri miaka inavyokwenda
wameshuhudia namna mahusiano hayo yanavyozidi kuwa imara na tija kwa
wananchi wa mataifa hayo.
Mbali
na taasisi zinazohusika na masuala ya wanawake na afya moja ya asasi
iliyoingia makubaliano hayo ya kuleta maendeleo ya pamoja kwa wanajamii
wa China na Tanzania ni Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji (SUKOS)
iliyochini ya Mstaafu, Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam
Suleiman Kova.
Balozi wa China nchini Tanzania Wang Ke (kushoto)
akimuongoza njia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job
Yusto Ndugai (katikati) Mara baada ya kuzindua rasmi ushirikiano wa
maendeleo ya pamoja kupitia asasi za kiraia, leo jijini Dar es Salaam.
Mstaafu
Kamanda wa Kanda maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova (aliyeketi
kushoto) akisaini makubaliano ya ushirikiano wa kimaendeleo kupitia
asasi za kiraia za nchini za Tanzania na China, leo jijini Dar es
Salaam.
Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Yustino
Ndugai akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Spika wa Jumuiya ya watu wa
China Ji Bingxuan, Balozi wa China nchini Wang Ke, Balozi wa Tanzania
nchini China Mbelwa Kairuki pamoja na viongozi wa asasi za kiraia kutoka
nchini China na Tanzania baada ya kuzindua rasmi ushirikiano wa kuleta
maendeleo ya pamoja baina ya mataifa hayo kupitia asasi za kiraia, leo
jijini Dar es Salaam.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job
Yusto Ndugai (kushoto) akibadilishana mawazo na Naibu Spika wa Bunge la
Jumuiya wa watu wa China Ji Bingxuan (katikati) kulia ni Balozi wa China
nchini Wang Ke.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...