Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (kushoto) akisaini kitabu cha Wageni alipokutana kwa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Chen Xiaoding (kulia) jijini Beijing, China Desemba 11, 2019. Dkt. Mnyepe yupo nchini humo kushiriki Mkutano wa Pili wa Jukwaa la Haki za Binadamu kwa Nchi zinazoendelea.

Dkt. Mnyepe amemuhakikishia Mhe. Chen kuwa, Tanzania itaendelea kudumisha ushirikiano na China kupitia Jukwa la Ushirikiano kati ya Afrika na China (Forum on China-Africa Cooperation - FOCAC). Aidha, kwa pamoja wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha kuwa, mageuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yanakuwa na tija kwa chi zinazoendelea hususan nchi za Afrika.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (kushoto) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Chen Xiaoding wakiwa katika picha ya pamoja jijini Beijing, China.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Chen Xiaoding walipokutana kwa mazungumzo jijini Beijing, China Desemba 11, 2019

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...