*******************************
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji K. Mnyepe ametoa msimamo huo wa Serikali alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Bw. George Kuchio katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Aidha, Dkt. Mnyepe ameitaka UNHCR kuzingatia na kuheshimu makubaliano baina yake na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1991 hususani Ibara ya Pili na ya Tatu (Articles II & III). Ibara hizo zinaelekeza kwamba UNHCR ni lazima ishirikiane
  na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutekeleza majukumu yake hapa Nchini.

Hivi karibuni UNHCR ililitaka Shirika la Msalaba mwekendu Tanzania (TRCS) kukabidhi majukumu yao bila kuihusisha serikali. Hatua hiyo ya UNHCR inavunja makubaliano ya 1991.

Hivyo amewaeleza UNHCR kwamba Shirika la Msalaba mwekundu Tanzania kuendelea na majukumu yake kwa kuzingatia makubaliano yaliyopo mpaka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na UNHCR watakapokubaliana vinginevyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...