Makundi 
yaliopo ndani ya chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha yanasababishwa na 
baadhi ya viongozi ambao sio waadilifu katika chama hicho mkoani Arusha
Hayo yameelezwa na katibu wa Itikadi na Uenezi taifa Wa chama cha mapinduzi  Hamphrey Polepole 
 ambaye pia ni mlezi wa CCM Mkoa wa Arusha wakati akiongea na wajumbe 
Wala chama cha mapinduzi mkoa Wa Arusha wakati katika mkutano maalumu Wa
 uchaguzi Wa Mwenyekiti Wa CCM mkoa ambapo alisema kuwa makundi yaliopo 
ndani ya chama hicho yanasababishwa na baadhi ya viongozi Wa serikali na
 chama wasio waadilifu 
Alisema
 wanachama Wa chama hicho hawana makundi  wala magenge ,ila baadhi ya 
viongozi ambao sio waadilifu,wasiotaka kutekeleza ilani ya chama cha 
mapinduzi, wanaoweka maslayi yao mbele badala ya maslayi ya chama ndio 
wanaunda makundi na kutengeneza magenge ya kuboma chama badala ya 
kujenga.
"Niwaombe  wana 
Arusha tuache makundi tukijenge chama chetu,tusikubali baadhi ya 
viongozi wasiokitakia chama chetu mema wakawatengenezea makundi ndani ya
 chama nataka kuona Arusha yetu ikiwa tulivu ,ikiendelea kuwa ya 
kijani,majimbo yote yakiongozwa na CCM ,na serikali ikiendelea 
kuendeshwa na chama chetu na hii italetwa na umoja wetu,na sio makundi 
ya wanachama au viongozi" alisema Polepole
Alibainisha
 kuwa yeye kama mlezi Wa chama hicho mkoa Wa Arusha hatamfumbia macho 
kiongozi yeyote au mwanachama ambaye ataendekeza ,au ataongoza kuunda 
makundi katika chama hicho ,kwani wanataka makundi yaishe ili chama 
hicho kiweze kuendelea kuongoza serikali na kuwaletea wananchi 
maendeleo.
Kwa upande wake Mwenyekiti Wa CCM mkoa Wa Arusha  Zelothe Steven Zelothe alitoa
 massa 48 kwa viongozi pamoja na wanachama Wa chama hicho wale wenye 
makundi kuyavunja Mara moja kwani wasipofanya hivyo na wakabainika hatua
 Kali zitachukuliwa dhidi yao.
Alisema
 kuwa  Kazi kubwa ambayo anaifanya nikukijenga chama cha mapinduzi mkoa 
Wa Arusha ,kuyafuta Makundi na makambi yote ambayo yapo ndani ya chama 
hicho ,kwani kwakufanya ivyo atajenga chama imara chenye wanachama imara
 watakayo weza kuilinda na kuiongoza nchi.
"Makundi
 na makambi yanaleta msuguano kwenye maofisi,kusengenyana   had I 
kupelekea kazi kitofanyika vizuri lakini Mimi sitakubali jambo hilo 
litokee kwakweli "Zelothe
Alibainisha
 amejipanga kushirikiana na idara zote za serikali,taasisi binafsi 
,viongozi Wa dini ,wananchi wote bila kuchagua hali yake kiuchumi ,huku 
akisisitiza kuwa atawapa ushirikiano zaidi wanyonge  kwa kutatua kero 
zao,atasimamia na kutatua kero za wananchi  na hii itasaidia kuendelea 
kujenga chama hicho.
Naye
 kada Wa Ccm aliejitambulisha  kwa jina LA Tausi Swalehe alisema ni 
kweli wanachama Wachama hicho hawana makundi ila kunabaadhi ya viongozi 
ambao sio waadilifu ndio wanatengeneza makundi ndani ya chama hicho.
Alibainisha
 kuwa nivyema wakaacha Mara moja tabia hiyo na kuanza kuwa pamoja na 
kujenga chama kimoja kitakacho waletea wananchi maendele



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...