Na, Editha Edward -Tabora

Wananchi mkoani Tabora wametakiwa Kujiunga na mfuko wa afya ya jamii Iliyoboreshwa (CHF) jambo ambapo litawasaidia kupata huduma ya afya kwa bei nafuu ya shilingi elfu thelathini kwa kila Maya watu sita

Ameyaeleza hayo mkuu wa mkoa huo Aggrey Mwanri wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kuwasisitiza wananchi Kujiunga na mfuko huo wa afya na kuwahakikishia upatikanaji wa dawa

Mwanri amesema mfuko huo utawasaidia wananchi wenye kipato cha chini kuweza kupata huduma ya afya kila mahali hapa nchini ukitofautisha na zamani ambapo mwananchi alipokuwa akijiunga kwa ajili ya kupata huduma ya afya ndipo anapotibiwa

"Mtu yeyote unapojiunga na mfuko huwa afya ya  jamii Iliyoboreshwa utatibiwa nchi nzima uwe bodaboda mama ntiliye mjasiriamali mkulima na kila Mtu atapata dawa kulingana na maelezo ya daktari "Amesema Mwanri 

Aidha Mwanri ametoa onyo kwa watumishi ya sekta ya afya ambao watahusika kwa kukwamisha zoezi hili kwa kuwabugua watu walio jiandikisha hatua kali zitachukuliwa hasa kwa upande wa Rushwa kwani ni kinyume na maadili

Kwa upande wake Afisa ustawi wa jamii ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tabora Baraka Mackona amebainisha jinsi ya Kujiunga na mfuko huo kwa wananchi ni kufika katika serikali za mitaa  na kujiandikisha ili kupata huduma hiyo

Aidha jumla ya Kaya elfu sita zimeshajiunga na mfuko wa (CHF)  Iliyoboreshwa  kwa mkoa mzima wa Tabora na zinaendelea kufaidika na huduma zinazotolewa na mfuko huo.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na wananchi Kujiunga na mfuko wa afya ya jamii Iliyoboreshwa CHF.


Afisa ustawi wa jamii ofisi ya mkuu wa mkoa Baraka Mackona akizungumzia jinsi ya wananchi wakitaka Kujiunga na mfuko huo wa afya ya jamii Iliyoboreshwa CHF.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...