Tangu kuingia katika soko la Afrika Mwaka 2018,StarTimes  inajitahidi kufikia Malengo yake, ili Kuhakikisha kwamba  kila Familia ya Kiafrika inapata ,nafasi na uwezo wa kuangalia/Kutazama Televisheni ya Kidigitali.
Na hivi sasa StarTimes inatoa huduma kwa  watu takribani Milioni 30 katika Nchi 37. Ukuaji Huu mkubwa  umeifanya  StarTimes kua Muendeshaji mkubwa wa Runinga  Barani Afrika na pia katika kuhakikisha inaleta maudhui mazuri kwa wateja wake.
StarTimes imetoa kipaumbele kwa jamii katika  kuhakikisha inarudisha kile inachopata hasa katika kuwaunga mkono Taasisi zidizo  za kiserikali,Sekta ya Filamu Afrika.
Mwaka 2019 StarTimes ilitoa mchango wake  kwa Jamii:

UCHANGIAJI
 Kampuni ya StarTimes Ilichangia Polisi  vifaa vya Michezo ikiwemo Tshirt,hii ilikua  katika kuchangia jamii na kusaidia mahitaji mbalimbali.
Vile vile StarTimes ilichangia Elimu katika kampeni ya TOKOMEZA ZERO Kisarawe kiasi cha Shilingi Milioni 10 katika kusaidia Serikali kwenye jitihada za kuhakikisha inatokomeza Zero.
Pia iliweza  kuchangia kiasi cha Shilingi Milioni 4 kwenye Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Cardiac Institute at Muhimbili National Hospital,Pesa hizo zilitolewa kusaidia Matibabu pamoja na huduma nyingine kwa watoto wenye matatizo ya Moyo.

HUDUMA KWA JAMII
StarTimes iliweza kutembelea kituo cha watoto yatima kitwacho (CHAWAMA ) kilichopo Sinza ,na kuwapatia msaada  kiasi cha Shilingi Milioni 3.
Kwa Upande wa Tamthilia mwaka 2019 StarTimes iliweza kuleta Tamthilia ya Waaris yenye maudhui yaliyopendwa  na watazamaji Wengi na imejichukulia umaarufu sana ikifuatiwa na Wild Flower,Blood Sister na The queen of Flow.
UDHAMINI
Mwaka 2019,StarTimes waliweza kudhamini tamasha la wasafi lililofanyika katika mikoa mitano na kumalizikia jijini Dar es salaam,na ilifanikiwa kudhamini mashindanoo ya kusaka vipaji ya Bongo Star Search ambayo yalikwenda vizuri na kuhitimishwa vizuri.

MATUKIO
Startimes iliweza kufanya matamasha  ya kuleta wasanii wa tamthilia ya Ode to Joy  iliyofayika  katika Hotel ya  Hyatty iliyopo Posta jijini Dar es Salaam.
ni wasanii maaurfu sana nchini China,Tamthilia hii iliweza kufanyiwa tafsiri kwa lugha ya kiswahili

TUZO
Startimes imekabidhiwa TUZO  kutoka shirika la TACAIDS  Tanzania kwa kutambua mchango wao StarTimes nao wakatoa mchango wa shilingi Million 5 ilikusaidia  Serikali katika mapambano dhidi ya  kutokomeza virusi vya Ukimwi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...