**************************
NA MWAMVUA MWINYI, KISARAWE
NAIBU Waziri Wa
Nishati ,Subira Mgalu ametoa tahadhali kwa vishoka baadhi ya watumishi
REA ,ama shirika la umeme Tanesco kujiepusha na uuzaji wa miundombinu ya
umeme na vifaa mbalimbali ikiwemo nguzo .
Ameeleza ,endapo
atabainika yeyote kujihusisha na vitendo hivyo atachukuliwa hatua kali
za kisheria kwakuwa anarudisha nyuma juhudi za serikali na ni uhujumu
uchumi.
Akihitimisha ziara
yake ya kukagua maendeleo ya mradi wa Peri -Urban wilayani Kisarawe,
Subira alisema, msimamo wa serikali nguzo haziuzwi ,hata kama mtumishi
upo REA ama TANESCO .
Aidha Subira ,alitoa rai kwa wananchi wasithubutu kulipia nguzo au kufanya makubaliano yoyote nje ya utaratibu wa serikali .Akizungumzia suala la
vishoka wanaofoji vitambulisho ,alisema serikali pia imeweka msimamo
,endapo kuna mazingira hayo wananchi watoe ushirikiano ili kuwabaini
wahusika.
Aliomba vyombo vya
usalama vya ngazi husika kuliona hilo ni moja ya majukumu yao kubaini
vishoka wanaouza miundombinu mbalimbali na vifaa na kubaini mtumishi
yeyote atakaehusika.
Pamoja na hayo,Naibu
Waziri huyo alitaka maeneo ya taasisi za umma ikiwemo shule na viwanda
kupewa kipaombele kufikishiwa umeme na kumtaka mkandarasi aendane na
kasi inayoendana na muda aliopangiwa ili jamii iondokane na adha ya
kukosa huduma ya nishati ya umeme.
Nae diwani wa kata ya
Msimbu ,Mama Lilomo alifafanua, kata yake imeguswa na umeme eneo la
Homboza lakini bado kuna changamoto ya ukosefu wa umeme katika vitongoji
saba.
Kwa upande wake ,Mkuu
wa shule ya sekondari Christon ,August Minja alieleza kwamba, mradi huo
utakapokamilika na kufika shuleni hapo, itakuwa ni chachu ya kuinua
taaluma,pia aliipongeza serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wake
Rais John Magufuli kwa kuhakikisha umeme unafika pembezoni na miji na
vijijini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...