Kaimu Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Proches Patrick akizungumza na waandishi wa habari pamoja na Timu ya Maafisa Habari wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto walipotembelea Mamlaka hiyo kuangalia mafanikio ya miaka minne ya serikali ya awamu ya tano ikiwa Kampeni ya Tumeboresha sekta ya Afya iliyoratibiwa na Maafisa habari wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara.


Mkuu wa Msafara na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Gerald Chami akitoa maelezo kuhusiana na kampeni ya Tumeboresha sekta ya Afya kwa kuangalia mafanikio ya miaka minne ya serikali ya awamu ya tano.
Meneja wa Mawasiliano na Elimu kwa Umma Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Gaudensia Simwanza akitoa akizungumza kuhusiana na mamlaka hiyo namna inavyofanya kazi za udhibiti wa dawa nchini
Mkaguzi wa Dawa wa Kanda ya Kaskazini wa (TMDA) Titus Malulu akitoa maelezo kuhusiana na wanavyofatilia dawa zikiwa sokoni kwa kutumia maabara hamishika.
Meneja wa Mawasiliano na Elimu kwa Umma Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Gaudensia Simwanza akionesha maabara hamishika ambayo wanaweza kukagua dawa sehemu yeyote.
Picha ya pamoja ya Kaimu Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Proches Patrick na waandishi wa habari pamoja na Timu ya Maafisa Habari wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto walipotembelea Mamlaka hiyo kuangalia mafanikio ya miaka minne ya serikali ya awamu ya tano ikiwa Kampeni ya Tumeboresha sekta ya Afya iliyoratibiwa na Maafisa habari wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara.
 
Na Chalila Kibuda,Michuzi Blog, Arusha

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Kaskazini imesema katika kipindi cha miaka minne ya Rais Dk.John Magufuli imefanikiwa kukagua shehena 3,160 za dawa, vifaa tiba, vitendanishi kupitia vituo vya forodha vya Namanga, ,Holili ,Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro pamoja na Tarakea.

Hayo yalielezwa jana na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa Mamlaka hiyo Proches Patrick amesema kuwa katika ukaguzi huo ni mafanikio kwao kwani kunafanya dawa,vifaa tiba na vitandanishi kuwa salama na bora kwa kulinda afya za watumiaji

Patrick amesema katika utendaji wao wa kazi wamechunguza ubora,Usalama na ufanisi wa sampuli 243 za dawa, vifaa tiba na vitendanishi huku maeneo 5,531 yanayojihusisha na biashara za dawa ,vifaa tiba na vitendanishi vimekaguliwa pamoja na watendaji wa vituo vya afya 152 wamepatiwa mafanzo ya utoaji wa taarifa za madhara yatokanayo na matumizi ya dawa na vifaa tiba.

Amesema kwa kazi zote zilizofanyika ni mafanikio kwa kanda ya Kaskazini TMDA imefanikiwa kufanya kazi kwa kwa kutumia mfumo wa Kieletroniki unaowezesha utoaji wa huduma huduma ndani ya siku moja.

Patrick kuwa wakati walipokuwa hawana mifumu huo walikuwa wanatumia siku tatu kwa wanaohitaji kibali kusafiri na kufika katika ofisi za TMDA.

Patrick amesema kuwa licha ya kutoa vibali vya waingizaji dawa lakini wanafatilia dawa hizo katika soko ili kujiridhisha dawa zinazotumika ni zile zilizopewa kibali na mamlaka hiyo.

“TMDA ipo kulinda afya za wananchi kuhakikisha dawa wanzotumia zina ubora na ikitokea kuleta madha kwa wananchi dawa hiyo inaondoka katika soko mara moja”amesema Patrick

Patrick amesema kuwa TMDA baada ya kutoa vibali vya uingizaji dawa huwa wanafanya utafiti wa dawa hizo katika kuhakikisha wananchi wanapata dawa zenye ubora.

Hata hivyo amesema katika mikakati hiyo kwa kanda ya kaslazini wameweza kusajili kiwanda cha dawa za mifugo ambacho kitaanza hivi karibuni.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...