Serikali ya Japan kupitia balozi wake nchini Tanzania Mh. Goto Shinichi Februari 28,2020 jijini Dar es Salaam imeingia mikataba minne tofauti katika muendelezo wa kuendelea kuunga mkono huduma za kijamii katika vijiji mbalimbali nchini Tanzania.

Serikali hiyo ya Japan ikiwakilishwa na Balozi Goto Shinichi imeingia mkataba wa kusambaza magari ya wagonjwa katika hospitali ya KCMC wenye thamani ya dola za Kimarekani 52,996.

Mkataba mwengine ni pamoja na kusaidia mazingira ya elimu katika wilaya ya Meatu mkoani Simiyu wenye thamani ya dollar za Kimarekani 90,729 ikiwa na lengo ya kwenda kuboresha mazingira ya elimu wilayani humo.

Pia serikali ya Japan imeingia mkataba wa ukarabati wa majengo ya shule ya sekondari kizimkazi iliyopo kusini Unguja wenye thamani wa dola za kimarekani 129,596.

Aidha pia serikali hiyo ya Japan imeingia mkataba wa ujenzi wa maktaba ya kujifunzia katika mkoa wa Kilimanjaro wenye thamani ya dola za kimarekani 90,271.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...