Kusikitishwa na taarifa ya vitendo vya baadhi ya Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Mwananyamala kuwanyanyapaa na kuwasumbua Wagonjwa

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imesikitishwa na taarifa ya vitendo vinavyofanywa na baadhi ya Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Mwananyamala vya kuwanyanyapaa na kuwasumbua wagonjwa wanaoenda kupata matibabu kwa kuwataka wagonjwa hao kwenda kufanya vipimo vya Korona kabla ya kuanza kupata matibabu.

Tume imesikitishwa na jambo hilo kwa sababu kila mwananchi ana haki ya kufurahia haki ya afya kwa kupata matibabu mazuri na ya uhakika. Madaktari na Wauguzi wanapaswa kutambua kuwa sio kila Mgonjwa ana maambukizi ya Korona.

Tume inaamini vitendo vya namna hiyo ni ukiukwaji wa haki ya afya kwa wananchi, na vinaweza kusababisha wagonjwa kupoteza maisha.

Aidha, Tume inatoa pongezi nyingi kwa Waziri wa Afya, Mheshimiwa  Ummy Mwalimu kwa kuchukua hatua za haraka za kukemea vitendo hivyo vya baadhi ya Madaktari na Wauguzi ambavyo vinaweza kuchafua taswira nzuri ya sekta ya Afya na jitihada mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali.

Hata hivyo, Tume inaiomba  Serikali iendelee kuhakikisha hospitali zinaendelea kutoa huduma nzuri kwa Wagonjwa ili kuepusha malalamiko yasiyo ya lazima.

Mwisho, Tume inaiomba Serikali kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo cha vitendo hivyo vinavyofanywa na baadhi ya Madaktari na Wauguzi ili  kuvitafutia ufumbuzi wa haraka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...