Na Sixmund J. Begashe wa Makumbusho ya Taifa

Msanii maarifu Nguza Mbangu Viking maarufu kama "Babu Seya" na Mkewe Desderie P. Haule ambae pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Tanga, wamefanya Utali wa ndani mjini Songea kwa kuitembelea Makumbusho ya Maji Maji  kwa lengo la kujifunza urithi wa historia ya Vita vya  Maji Maji vilivyo tokea miaka ya 1905 hadi 1907.

Akizungumza baada ya kuitembelea Makumbusho hiyo Bw Viking ameipongeza Makumbusho ya Taifa kwa kuhifadhi urithi huo wa kihistoria kwani umempatia nafasi ya kujifunza kwa kuona namna mababu zetu walivyo tanguliza uzalendo katika kupigania haki na heshma yetu. 

"Nimejifunza mambo mengi, japo yanaumiza sana lakini yanatupa faraja na ujarisiri katika kuendelea kulinda heshma yetu kama watanzania, Mashujaa wa Maji Maji wamesha timiza wajibu wao sasa kazi ni kwetu hasa katika kuunga mkono jitihada za Mhe Rais wetu Dkt John Pombe Magufuli katika kuleta maendeleo nchini" Alisema Bw Viking.

Nae Mke wa Viking Bi Desderie Haule licha ya kufurahia Utalii huo wa ndani katika kipindi chake cha likizo alisema kuwa ipo haja hasa vijana kuitembelea Makumbusho hiyo ya Vita vya Maji Maji ili kujifunza, uzalendo, upendo, kujituma na mengineyo ambavyo ni misingi bora ya uongozi utakao nufaisha Taifa Leo kama tunavyo nufaika sasa kupitia Mhe Rais wetu ambae ni  Mzalendo  Dkt John Pombe Magufuli

Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho nchini Dkt Noel Lwoga ambae yupo Songea kikazi amekutana watalii hao wa ndani (Familia ya Babu Seya) na kuwapongeza kwa kuitembelea Makumbusho hiyo na kutoa wito kwa wakazi wa Ruvuma na wote wanao ingia Songea kwenda katika Makumbusho hiyo ili kujione na kujifunza historia hadhimu ya Taifa hili kupitia Vita vya Maji Maji.
 Msanii Nguli nchini na Mkewe Bw Nguza Mbangu Viking (Babu Seya) wakipata Maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Makumbusho ya Majimaji Songea Bw Erick Soko juu ya Historia ya Vita vya Majimaji.
  Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga wakiwapongeza Bw Viking na Mke wake Bi Desderia Haule kwa kuitembelea Makumbusho ya Majimaji Mjini Songea
Kulia Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho  ya Taifa Dkt Noel Lwoga akiongozana na Bw Viking na Mkewe wakitoka kuangalia Mnara wa Askari uliopo Makumbusho ya Maji Maji Mjini Songea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...