Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

 INAAMINIKA kuwa chimbuko la kusherekea siku za kumbukizi za  kuzaliwa maarufu kama 'Birthday' zilianzia barani Ulaya kabla hata ya kuanza kwa ukristo, katika imani ya kipagani iliaminika kwamba mapepo huwatembelea watu katika kumbukizi za siku zao za kuzaliwa, hivyo wakatumia siku za kuzaliwa kujumuika na ndugu na marafiki ili wasitembelewe na mashetani.

Katika imani hiyo ya kipagani iliamini imani za kishirikina katika sikukuu za kuzaliwa, waliamini kwamba mashetani huvutiwa sana na watu katika sikukuu zao za kuzaliwa "Birthday" kwahiyo watu wenye imani ya kipagani waliwalinda washerehekewa katika siku zao za kuzaliwa ambapo ndugu na marafiki waliwatembelea ili kuwakinga na madhara ya mashetani kwa kuwazunguka, kuwaombea heri pamoja na kupiga kelele kubwa kwa malengo ya kuwaogopesha na kuwakimbiza mashetani.

Baadaye ukaja utamaduni wa keki na kuwasha mishumaa ambapo baadhi ya watu waliamini kwamba utamaduni huo ulianzia kwa wagiriki ambao walitengeneza keki  yenye muundo wa mwezi na kuiweka katika hekalu la Armites (Mungu wa mwezi) na wengine waliamini utamaduni huo ulianzia kwa wajerumani ambao walitengeneza mkate ulio na umbo la mtoto Yesu akiwa na nguo za kitoto.

Kinachofahamika na wengi zaidi ni kwamba utamaduni wa keki na mishumaa umetokana na imani ya kidini ambao wengi huamini Mungu anaishi mawinguni na kupitia mishumaa inayowashwa husaidia kupeleka maombi na ishara kwa Mungu, huku Wajerumani wakiamini kuweka mshumaa mkubwa katikati ya keki huashiria "Mwanga wa Maisha."

Utamaduni wa kusherekea siku za kuzaliwa umeendelea hadi sasa ambapo wengi huweka heri zao kimoyomoyo pindi wanapozima mishumaa, na huaminika kuzima mishumaa yote kwa pumzi moja huleta bahati nzuri.

Unaamini nini katika kusherekea siku yako ya kuzaliwa? kula keki na kuzima mishumaa huwa unamaanisha nini?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...