Na Mwandishi Wetu, Babati
TAASISI
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Mkoani Manyara,
wanamtafuta mmiliki wa kampuni ya JACO Service Group, John Stepheni
Kabelinde (Babu Joha) kwa kujipatia isivyo halali kandarasi ya kufyeka
nyasi pembeni ya barabara.
Mkuu
wa TAKUKURU wa Mkoa wa Manyara, Holle Joseph Makungu ameyasema hayo
mjini Babati Julai 9 mwaka huu wakati akizungumza na waandishi wa
habari.
Makungu amesema
Kabelinde maarufu kwa jina la Babu Joha huonekana mara kwa mara maeneo
ya Sinza Makaburini jijini Dar es salaam ambapo inasadikiwa ndipo
anapoishi na kuendesha shughuli zake.
Amesema
wanamtafuta Babu Joha kwa sababu anatuhumiwa kujipatia kandarasi
inayohusu kufyeka nyasi pembeni mwa barabara inayotoka Babati hadi
Gehandu Mkoani Manyara.
Amesema
uchunguzi unaonyesha Babu Joha aliwasilisha nyaraka za kupotosha
zilizomuwezesha kuwashinda wazabuni wengine tisa walioomba kazi hiyo.
Amesema
uchunguzi unaonyesha Babu Joha kupitia kampuni yake ya JACO Service
Group amekuwa akikwepa kulipa kodi mbalimbali za serikali hivyo
kuangukia kwenye makosa ya kuhujumu uchumi wa Taifa.
"Ni
rai yangu kwa wananchi wa mkoa wa Manyara na watanzania wote kupitia
kwenu wana habari popote babu Joha atakapoonekana toeni taarifa kwa
ofisi za TAKUKURU zilizopo karibu nanyi au kupitia namba yetu ya dharura
ya 113 au kamanda wa TAKUKURU mkoani Manyara 07388150124-25," amesema
Makungu.
Amezionya
kamati za tathimini za taasisi za ununuzi kutimiza majukumu yao kwa
kuhakiki kila kampuni wanayoifanyia tathimini kuona uhalali wa nyaraka
zilizowasilishwa na kujiridhisha iwapo kampuni husika inalipa kodi za
Serikali.
"Kushindwa
kufanya hivyo ni matumizi mabaya ya madaraka kinyume cha k/f cha sheria
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11/2007 na hatua zitachukuliwa
dhidi ya wahusika," amesema Makungu.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...