Na Woinde Shiza, Michuzi Tv ARUSHA

MGOMBEA  urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ) Tundu Lissu  pamoja na Mgombea Mwenza wake Salim Mwalimu   wanatarajia kuingia mkoani Arusha Agosti 14 ,2020 mkwa ajili yakusaka wadhamini   katika mikoa ya Kanda ya Kaskazini

Hayo yamebainishwa na  Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini   ambaye pia alikuwa Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema alipokuwa akizungumza  na waandishi wa habari ambapo amebainisha wanatarajia kumpokea mgombea huyo wa urais na mgombea mwenza wake katika kiwanja cha ndege cha Arusha.

Amesema wagombea hao wanakuja mkoani Arusha kwa ajili ya uthamini wa fomu  ya ugombea  Urais ,ambapo amewataka wanachama wote wa CHADEMA  kujitokeza kwa wingi ,pamoja na viongozi wote wa kanda kujitokeza kumpokea.

‘’Baada ya kumpokea tutakuja naye na wananchama pamoja na viongozi wa Chama waliojitokeza kumleta mpaka ofisini na kufanya  mkutan mfupi kwa ajili ya kumdhamini na hutuba fupi itakuwepo hapo na mgombea wetu ataondoka na kuelekea katika maeneo mengine na tayari ratiba zimeshatolewa na maelekezo ya kiofisi.

"Wanachama wetu wajiandae tu kwa ugeni huo,niwatake tu wananchi wajitokeze kwa wingi kuja kumthamini mgombea na safari hii sisi kama chadema tumejipanga kupeleka  zaidi ya  idadi ya wadhamini ambao Tume wamependekeza,"amesema Lema

Wakati huo huo mchakato kuchukua fomu ya kugombea nafasi za ubunge na udiwani kwa chama hicho kwa upande wa Kanda ya Kaskazini umeaanza leo na wanachama wameshaanza kuchukuwa fomu   ila yeye hatachukuwa fomu wiki hii.

Bali atatangaza rasmi siku ambayo atachukuwa fomu ,na yeye ndie mgombea ubunge jimbo la Arusha Mjini na hatagemei Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC)waseme kuna mgombea mwngine wa Chadema  atakayesimama jimbo la Arusha Mini  .

“Tunaendelea kuangalia jinsi uchukuaji wa fomu unavyoenda  na tuna watu kila upande  wanafatilia suala hili  kila mahali na niseme hatutakubali matendo maovu yaliyofanywa  kipindi cha uchaguzi wa Serikali za mitaa ujirudie kipindi hiki,"amesema.

Ametoa mwito kwa Jeshi la Polisi kuendelea kutiii sheria bila shuruti ,kama vile wanavyowaelekeza  wananchi kutii sheria bila shuruti huku akiwataka wandelee kuwa wapole kama vile walivyoanza mwanzo.
Mwenyekiti wa CHADEMA  kanda ya kaskazini ambaye pia alikuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema  akizungumza leo katika ofisi za kanda za chama hicho mblele ya Waandishi wa habari ambapo alibainisha kuwa wanatarajia kumpokea mgombea huyo wa urais pamoja na mgombea mwenza wake katika kiwanja cha ndege cha Arusha ambapo alisema watakutana katika mzunguko wa kisongo (picha na Woinde Shizza,Arusha )

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...