NA MWAMVUA MWINYI,CHALINZE
JESHI la polisi mkoani Pwani, linawashikilia wahamiaji haramu (wanaume), kutoka nchini Ethiopia wapatao 5, kwa kosa la kuingia nchini bila kibali .
Kamanda wa polisi mkoani humo,Wankyo Nyigesa alithibitisha juu ya tukio hilo ambapo alisema ,huko eneo la Mzani wa magari Msata, Chalinze, polisi wakiwa doria barabara kuu ya Chalinze kuelekea Tanga ,lilikamata gari namba T.246 BBG aina ya scania tani 10 ,hard top .
Alieleza ,gari hilo lilipopekuliwa lilikutwa likiwa na raia 51 wote wanaume wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 15-25 ambao walikuwa wanasafirishwa kutoka Tanga -kuelekea Chalinze kupitia Msata na watu wawili wanaodhaniwa kuwa waTanzania ambao walitoka ndani ya gari na kukimbia .
Wankyo alibainisha gari hilo linaonyesha linamililiwa na Uswege Mwamboma ,wa Tukuyu Mbeya .
Kamanda huyo aliwataka mmiliki wa gari na ambao wamehusika kuwasafirisha wahamiaji hao haramu kujisalimisha wenyewe kabla hawajatiwa nguvuni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...