Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Dkt Maduhu Kazi amekadhi serikalini shule mbili zilizojengwa na mwekezaji wa Alliance Ginnery katika vijiji vya Salama na Bugatu kwa upande wa Sekondari na Kijiji cha Kasoli kwa upande wa chuo cha ufundi stadi.
Shule hizo zilikabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Magu Mh. Salum Kali ambaye alipokea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mh. Anthony Mtaka kwa upande wa shule ya ufundi.
Dkt. Maduhu Kazi amewapongeza wawekezaji hao kwa moyo wao wa kurudisha shukran kwa wananchi kwa kufanya maendeleo kwa wananchi.
Naye Mh. Mtaka amemshukuru Mwekezaji na kusema Mwekezaji huyu ni wa kipekee na amekuwa na mchango mkubwa kwa maendeleo ya vijiji vingi vya Simiyu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...