Vyombo vya ulinzi na usalama Mkoa wa Dar es salaam vimefanikiwa kuwatia mbaroni Wahamiaji haramu 36 raia wa Ethiopia na Somalia walioingia nchini kinyume na taratibu ambapo Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Aboubakar Kunenge ametoa onyo Kali kwa Raia wa Tanzania wanaoshiriki kuwafadhili na kuwasafirisha kwa ili wapate fedha.

RC Kunenge amesema Wahamiaji hao walikamatwa usiku wa kuamkia November 15 kwenye fukwe za Mbweni ambapo kati yao 30 wanatoka nchini Ethiopia na Sita wanatokea nchini Somalia.

Aidha RC Kunenge amesema hata utaratibu unaotumika kusafirisha watu hao unakiuka Sheria, haki na utu wa binadamu sababu wengi wao wanafungiwa kwenye kontena zisizokuwa na hewa na pindi wanapobainika kufariki Dunia maiti zao hutupwa kwenye vichaka.

Pamoja na hayo RC Kunenge amevipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya.

Kwa upande wake Afisa uhamiaji Mkoa wa Dar Es Salaam Kamishina Msaidizi Edmund Mrosso amesema kinachofuata baada ya wahamiaji hao kukamatwa watafikishwa Mahakamani kwa kosa la Kuingia nchini kinyume na taratibu.

Aidha Kamishina Mroso amesema kwa wale wanaowasafirisha au kuwahifadhi wahamihaji hao adhabu inaelekeza kifungo Cha miaka 20, faini ya shilingi milioni 20 au vyote kwa pamoja ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali zilizotumika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...