Na Mwandishi wetu, globu ya jamii

KUELEKEA msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka Jeshi la Zimamoto na uokoaji hapa ncini latoa tahadhari ili kusitokee matukio yatakayo athiri afya za wanajamii.

Jeshi hilo linajulisha umma kwa ujumla kuwa katika kipindi hiki cha Sikukuu za Krismas 2020 na Mwaka mpya 2021, litahakikisha maeneo yote yapo salama zikiwemo nyumba za ibada, fukwe na kumbi za starehe.

Katika Taarifa yake iliyotolewa na jeshi hilo imesema kuwa Wamiliki wa Kumbi za Starehe wahakikishe kuwa kumbi zao zimekaguliwa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na zimewekwa mifumo na vifaa vya kuzima moto, ili kuzuia majanga ya moto, kumbi ambazo hazitakidhi usalama hazitaruhusiwa kutumika.

"Wamiliki wa vyombo vya Usafiri na Usafirishaji na Madereva, pamoja na kuzingatia sheria zote za usalama barabarani, wanatakiwa kuwa na vizima moto kwenye magari yao." Imesema Taarifa hiyo.

Aidha Wazazi wanatakiwa kutowaacha Watoto wao na wenye mahitaji maalum peke yao, wanapokuwa kwenye matembezi bila ya kuwa na uangalizi wa karibu. Tunatoa rai kwa wananchi wanaotumia mapambo (Taa) ya krismas na mwaka mpya yanaweza kusababisha moto wachukue tahadhari ya hali ya juu.

Kwa huduma ya haraka juu ya majanga ya moto na maokozi Piga namba 114.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...