Msikilize Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT-CCM) Mkoa wa Dodoma, Neema Majule akielezea mambo mbalimbali ikiwemo jinsi uongozi wake ulivyowezesha ujenzi wa miradi miwili ya Shule ya Awali na jengo la maduka Kilimani, jijini Dodoma, na mipango mingine ya ujenzi katika viwanja vyao 6 walivyovikomboa baada ya kudhurumiwa.
Pia mama huyo jabali, amewapongeza wanawake kwa kufanikisha ushindi mkubwa wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. Vilevile ameupongeza uongozi wa juu wa chama hicho kinachoongozwa na Rais John Magufuli kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa miaka mitano ya kuiletea Tanzania mafanikio jambo ambalo pia limechangia CCM kupata ushindi mkubwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...