Na Muhidin Amri,Songea

WANANCHI wa kijiji cha Mgazini kata ya Mgazini halmashauri ya wilaya Songea mkoani Ruvuma,wameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuongeza idadi ya watumishi  wa sekta ya Afya na dawa katika zahanati ya kijiji hicho ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa watumishi na dawa.

Hayo yameelezwa jana na baadhi ya wananchi wa kijiji hicho waliohudhuria mkutano wa kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi  juu ya ufuatiliaji  wa Uwajibikaji jamii uliofanywa na shirika lisilo la kiserikali  ROA kupitia mradi wa SAM unaofanya kazi katika sekta ya Afya kwenye kata tano za wilaya ya Songea.

Lucius Bula na Damian Mwenda wamesema, katika zahanati  ya kijiji hicho kuna mganga mmoja na wauguzi watatu,hivyo kutokana na idadi kubwa ya watu  inakuwa vigumu kwa watumishi hao kutoa huduma kwa  wakati muafaka na kusababisha  wagonjwa kutumia muda mwingi  wakiwa foleni ya kuonana na Daktari.

Bula alisema,kwa sasa idadi ya watumishi  waliopo ni ndogo kufuatia  watu  wengi hasa wageni wanaofika katika kijiji hicho na mikoa  mingine hapa nchini kwa ajili ya shughuli mbalimbali kama kilimo na ufugaji ambao  pindi wanapougua wanakimbilia zahanati ya Mgazini kupata huduma ya matibabu.

Kwa mujibu wa Bula,kuingia kwa wageni hao  kumesababisha watumishi hao kuzidiwa na idadi ya wagonjwa na hivyo kusababisha baadhi  ya wananchi kukimbilia  Hospitali ya St Joseph Peramiho na wengine Hospitali ya mkoa Songea umbali wa km 45.

Damian Mwenda amesema, awali zahanati hiyo ilijengwa kuhudumia wananchi wa Mgazini tu, lakini  sasa  inalazimika kuhudumia wananchi wa vijiji vya jirani na ndiyo maana hata dawa zinazoletwa hazitoshelezi, kwa kuwa serikali inapeleka dawa kwa ajili ya  kuhudumia wananchi  wa kijiji kimoja  na sio wa vijiji vingine.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...