Diwani wa Kata ya Arusha Chini Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro, Leonard Waziri Mkakanzi, Leo Januari 19,2010 amekabidhi tani tano za mahindi katika shule tisa zilizopo kwenye Kata yake ikiwa ni sehemu ya mchango wake katika kusaidia elimu kwenye shule zilizopo katika Kata yake yenye wanafunzi takribani elfu tatu mia saba (3700)
Diwani wa kata ya Arusha Chini mkoa wa Kilimanjaro, Leonard Mkakanzi kulia, akikabidhi mahindi kwa ajili ya chakula kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi ya Kiyungi Mpya, Marry Malimbwi, na kushoto ni Diwani wa Kata ya Kahe Mashariki Kulwa Kamili Mmbando ambaye pia ni mwenyekiti wa mipango halmashauri ya wilaya ya Moshi.Wanafunzi wa shule ya msingi Kiyungi kata ya Arusha Chini mkoani Kilimanjaro wakipokea mahindi kutoka kwa Diwani wa Kata hiyo, Leonard Mkakanzi kwa aili ya chakula cha shuleni hapo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...