Mkuu wa Wilaya Ya Arusha Mh Kenani Kihongosi ameongoza jogging leo akiwa na wananchi wa Jiji la Arusha, amesisitiza Umoja Amani na Utulivu pia wananchi kujitolea kushiriki katika shughuli za Kizalendo.

Pia Mhe Kenani Kihongosi ameishukuru kampuni ya ASAS DIARIES MILK kwa sapoti kubwa yamaendeleo inayotoa kwa wananchi ikiwemo Ajira na huduma za Kijamii, amesema watazidi kuwaunga mkono kwani wanafanya kazi nzuri kwa jamii.

Amewashukuru wananchi wa Jiji la Arusha kwa namna ya kipekee na Amewaeleza atazidi kuwatumikia kwa nguvu zote bila kuchoka.

Mwisho Amempongeza na Kumshukuru Mh Rais Dr. JOHN POMBE MAGUFULI kwa Kuwaletea maendeleo makubwa wananchi wa Jiji La Arusha na amesema wananchi wazidi kushirikiana na Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuchapa kazi kwa bidii kwani Mheshimiwa Rais Ameonyesha Nia ya dhati ya Kuibadilisha Tanzania kiuchumi hivyo lazima tumuunge Mkono.

Mtumishi wa Wote








 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...