MTEGO uliowekwa na  Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA) Kanda ya Kusini umefanikiwa kumnasa Jamaly Sad akiuza dawa za Serikali.

Taarifa ya TMDA inaeleza kwamba Sad amenaswa kwenye mtego huo Januari 31 ,2021 wilayani Newala na alikuwa akiuza dawa za Serikali za Mpango wa Uzazi.

Dawa hizo ni Medroxy Progesterone (vichupa 60) na Microgynon pills (vidonge 3360) zote zikiwa na thamani ya Sh. 300,000.

Hivyo kwa sasa Sad na mtoto wake wanatuhumiwa kuuza dawa hizo za Serikali na wamefunguliwa jalada polisi RB No.NL/RB/94/221 na yuko ndani kwa hatua zaidi kisheria. 

Mtuhumiwa Jamaly Sad akiwa dukani kwake


 

 

 

 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...